Jumanne, 17 Mei 2016

Wakuu wa mikoa wapewa changamoto

sm5Makamu wa Rais wa Jamhuri uya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akikabidhi Hundi kwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Chiku Galawa kwa ajili ya kukabiliana na uhaba wa Madawati. Jumla ya  Madawati Elfu 16.5 yenye thamani ya Tshs. 1 Bilioni moja zilikabidhiwa kwa Wakuu wa Mikoa inayozunguka Mbuga ya Hifadhi ya Taifa kwa ajili yakukabiliana na tatizo la Madawati kwenye Shule zote zilizomo katika Wilaya za Mkoa hiyo. Makabidhiano hayo yamefanyika leo Mei 16,2016 katika ukumbi wa Ngurudoto mjini Arusha.katikati waziri wa Maliasili Utalii Profesa Jumanne Magembe.
…………………………………………………………………………………………..
Mahmoud Ahmad Arusha
Wakuu wa mikoa hapa nchini wametakiwa kuanza kutenga maeneo ya malisho ya mifugo kwenye mikoa yao kuepuka mifugo kuingia kwenye hifadhi za taifa na atakayeshindwa kwenda na maji.
Kauli hiyo imetolewa na makamu wa raisi Samia Suluhu Hassan wakati akikabidhi madawati kwa wakuu wa mikoa 19 na wilaya 55 za hapa nchini yaliotolewa na mamlaka ya hifadhi za taifa Tanapa jijini Arusha.
Alisema kuwa umefika wakati kwa mikoa iliyokaribu na hifadhi za taifa kuanza kuwadhibiti wafugaji wanaoingiza mifugo katika hifadhi kwa kisingizio cha kutokuwa na maeneo ya malisho kuanza mkakati wa kutenga maeneo ilikuokoa mazingira na uoto wa asili.
Amewataka wakuu hao wa mikoa kuwa na ukaribu na wahifadhi katika maeneo yao jambo litakalosaidi kuhifadhi ikolojia ya maeneo ambayo yamekuwa chachu ya kuchangia pato la taifa.
“Kwa Mkuu yeyote atakayeshindwa katika hili ajiandae kutumbuliwa jipu kwani hakutakuwa na msamaha katika hili”alisisitiza  makamu wa raisi.
Amesema kuwa msaada huo uliotolewa uwe chachu ya mabadiliko katika kuhakikisha wanafunzi wanapata Elimu stahiki bila usimbufu wa kukaa chini na kuweza kuleta tija katika masomo.
Awali akimkaribisha makamu wa raising kuongea waziri wa maliasili na utalii Jumanne maghembe alisema kuwa imekuwa kawaida ya ujirani mwema kati ya hifadhi za taiga na vijiji kurudisha faida katika miradi inayoibuliwa na wananchi ikiwemo changamoto ya ukosefu wa madawati na madarasa katika vijiji vinavyopakana hifadhi zetu za taifa note nchini.
Alisema kutokana na changamoto hiyo ya kufanikisha upatikanaji wa Elimu bure kwa wanafunzi kuingia shuleni kwa wingi na kuwa na changamoto ya ukosefu wa madawati nipo wizara kupitia tanapa wakaja na mkakati huo wa madawati.
Nae mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo Allan Kijazi alisema kuwa shirika hill litatoa madawati 500 kwa wilaya 55 katika mikoa 19 ya hapa nchini ambapo mingi inapitiwa na hifadhi zetu za taifa.
Amesema lengo kuu in katika dhana nzima ya ujirani mwema ilikuondoa changamoto mbalimbali kati ya hifadhi na jirani zao katika kuhakikisha mipaka na uikolokia unaendelea kuwepo.

0 maoni:

Chapisha Maoni