Jumanne, 17 Mei 2016

Wanafunzi wa shule ya Msingi Ishololo Kata ya Usule Jimbo la Sorwa Shinyanga wakohatarini kupata maradhi ya mlipuko

shule zetuNa Masanja Mabula –Shinyanga
 WANAFUNZI wa shule ya Msingi Ishololo Kata ya Usule Jimbo la Sorwa Halmashauri ya Shinyanga Vijijini  wako hatarini kupata maradhi ya kuambukiza , kutokana na Shule hiyo kukosa choo kwa kipindi cha miaka mitatu sasa .
Shule hiyo yenye wanafunzi zaidi ya mia nne (400) wa darasa la kwanza hadi la saba ambao wanatumia vichaka vilivyoizunguka Shule hiyo  kama choo , jambo ambalo linaweza kusababisha madhara ya kupata magonjwa ya mripuko ikiwemo kipindi kipindu.
Wakizungumza na mwanadishi wa habari hizi , baadhi ya wazazi wa wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo , walisema bado uongozi wa kijiji pamoja na kamati ya shule hawajalipa kipaombele suala la ujenzi wa Choo katika Shule hiyo.
Aidha waliutaka uongozi wa Serikali ya kijiji kuweka wazi matumizi ya michango ya wazazi ambao walichangia kila familia Tshs 2,500/=ambazo hadi sasa hawafahamu jinsi zilivyotumika kwani tatizo liko pale pale .
Mmoja wa wanakijiji aliyejitambulisha kwa jina la Kurwa Shija aliliambia gazeti hili kuwa uongozi wa kijiji pamoja na kamati ya shule wameshindwa kufafanua sababu zilizokwamisha ujenzi wa choo licha ya kwamba wazazi walichangia mamilioni ya fedha kwa ajili ya kuliondoa tatizo hilo.
“Kijiji kina familia zaidi ya mia nne , na kila familia ilichangia Tshs 2,500/= miaka mitatu iliyopita , lakini  hatujui ni sababu gani zimekwamisha ujenzi wa choo , tuna wasiwasi  watoto wetu kupata maradhi ya mripuko ”alifahamisha.
Naye John Salamba akizungumza kwa masikitiko alifahamisha tatizo hilo lilisababisha baadhi ya wazazi kufikishwa mahakamani baada ya kukaidi agizo la kuchangia 2,500/= kama walivyokubaliana .
Aidha aliutaka uongozi wa Kijiji kuitisha mkutano wa wanakijiji wote ili kujadili hatma ya ujenzi wa Choo , ambao umekwamba bila ya kutolewa taarifa sahihi  na sababu zilizokwamisha kuanza kwa ujenzi huo.
“Uongozi wa Kijiji uliwahi kuwafikisha mahakamani baadhi ya wanakijiji wakati wa uchangiaji , lakini kwa sasa hatuoni kinachoendelea , hivyo iko haja kwa serikali ya kijiji kuitisha mkutano ili watueleze wapi walipokwama ”alisema.
Wakizungumzia kadhia ya ukosefu wa choo , baadhi ya wanafunzi walielezea hofu juu ya  usalama wao na  maisha yao , na kuutaka uongozi wa Kijiji na Kamati ya Shule kuharakisha ujenzi wa Choo ili waondokane na adha ya kutumia vichaka kujisaidia.
Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji Juma Panya pamoja na Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo hawakupatikana kulizungumzia hilo baada ya kudai kwamba wako nje ya Kijiji kikazi na kutaka watafutwe siku nyin

0 maoni:

Chapisha Maoni