Jumatano, 25 Mei 2016

COSATO CHUMI AKABIDHI GARI LA WAGONJWA HOSPITAL YA MAFINGA


MBUNGE wa Jimbo la majinga   Mjini, Cosato Chumi akikabidhi gari la Wagonjwa
(ambulance) kwa wananchi


Gari la wagonjwa [Ambulance] lenye thamani ya mill.40 lakabidhiwa katika Hospitali ya wilaya ya mafinga na mbunge wa jimbo la mafinga mjini Cosato Chumi katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana kwenye viwanja vya mashujaa mjini mafinga mkoani Iringa.
Chumi  alikabidhi gari hilo ikiwa ni moja ya ahadi yake alyoitoa wakati akiomba kura kwa wananchi wa jimbo hilo katika kampeni ya uchaguzi mkuu 2015,ambapo alisema kutokana na changamoto ya uhaba wa gari ya kubebea wagonjwa katika hosipitali hiyo, endapo atapewa  ya kuwa mbunge atahakikisaha gari ya wagonjwa linapatikanaili wagonjwa waweze kufika hospital kwa wakati.
Akizungumza na wananchi wakati wa kukabidhi gari hilo,mbunge  Chumi alisema muda wa kupiga siasa umeshapita na kazi iliyopo hivi sasa ni kuwaletea wananchi maendeleo kwa kuwatatulia changamoto zinazowakabili.
Alisema pamoja na kuongeza gari ya wagonjwa atahakikisha anaboresha vituo vya Afya  vilivyopo katika jimbo lake ili kupunguza wimbi kubwa la msongamano wa wagonjwa wanaokuja kutibiwa Hospitalini hapo.
‘’’Nipo kwenye mchakato wa kuboresha vituo vyote vya Afya ndani ya jimbo langu,na nitahakikisha huduma muhimu zinapatikanaikiwa pamoja na dawa za kutosha na vifaa mbalimbali vinavyohitajika ili wananchi wangu waweze kuhudumiwa bila usumbufu katika vituo hivyo,hii itasaidia kupunguza msongamano katika hospitali ya wilaya’’’’’alisema chumi
Aidhakatika mkutano huo mbunge alisisitiza swala la uaminifu kwa watumishi waliopewa dhamana ya kuwatumikia wananchi wahakikishe wanajikinga na  vitendo vinavyoashiria rushwa ,vinavyoweza kuwaharibia sifa ya utendaji kazi zao na kushindwa kuwajibika ipasavyo katika majukumu yao.
‘’’Sisi wabunge,madiwani na mtumishi yeyote aliyepewa dhamana na wananchi anatakiwa ajiepushe na swala zima la rushwa ili aweze kutenda haki kwa kuwatatulia changamoto wananchi wake waliomchagua.       Tunatakiwa tuwatumie wananchi kuwaletea maendeleo  ipasavyo na si vinginevyo’’’alisema
Innocent Mhagama ni kaimu Mganga mkuu wa Hospitali ya Wilaya  mafinga,akipokea msaada wa gari hilo kutoka kwa mbunge Chumi alisema gari hilo litaweza  kusaidia kuokoa vifo vya wanamafinga hasa mama na mtoto ambapo hapo awali kuliwa na gari moja tu.
Mhagama alisema kutokana na uwingi wa wagonjwa wanaoenda kutibiwa katika hospitali hiyo kwa mwezi ni zaidi ya500 aliosimia kubwa ni akina mama wajawazito na wengi wao wanafikishwa wakiwa katika hali mbaya  kutokana  na gari la wagonjwa kuwa moja na kushindwa kumudu.
‘’’’Hospitali ilikuwa na gari moja tu la wagonjwa ambalo lilikuwa linahudumia zaidi ya vituo 19 vilivyopo.Tunamshukuru mbunge kwa kuliona hili na na kuokoa maisha ya watu hasa mama na mtotoingawa bado hitaji lipo kutokana na uwingi wa wagonjwa  endapo tutapata gari la tatu  itasaidia sana’’’’’alisema
Wananchi nao walitoa malalamiko yao kwa mbunge Chumi,ambapo Maria Kanyika alimuomba mbunge aweze kusiomamia swala la utapikananji wa vibali vya kuvuna miti,kwa kumtaka ahakikishe wazawa wa eneo husika wanapewa kipaumbele ili waweze kunufaika mali alisi hiyo ilipo kwako.
‘’’’Tumelia kwa muda mrefu,sisi tunanyanyasika kwa kuwapendelea wageni na kutuacha sisi wenyeji tuliopo hapa.Nimeomba mara tano hivi sasa na ukizingatia mimi ni mjane lakini naachwa  na pesa yangu inaliwa wageni wanapewa hali inayotukatisha tama wananchi tuliouzunguka msitu huu.’’’’alisema


0 maoni:

Chapisha Maoni