Jumanne, 24 Mei 2016

HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA YAKUSANYA TSH 9,278,106,404 KWA KIPINDI CHA MIEZIMITATU

Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imewataka wakazi wa Mji huo kulipa kodi ya majengo na ushuru wa manispoaa hiyo kwa hiyari ili kuinua uchumi wa Halmashuari hiyo inayojipanga kufikia hadhi ya kuwa jiji
Kauli hiyo ilitolewa Meya wa Manispaa hiyo Alex Kimbe alipokuwa akifunga kikao cha baraza la madiwani kilichokuwa kikipokea taarifa za roba ya tatu ya mwaka kilichofanyika juzi  kwenye ukumbi wa Mansipaa hiyo mjini hapa.
Kimbe alisema kwa kipindi cha mizei mitatu Halmashauri hiyo imekusanya Sh 9,278,106,404 kati ya makisio ya kukusanya sh 11,278,561,183,kwa kipndi cha miezi mitatu.
“Sisi Manispaa tumefanya uthamani wa Majengo yote na niwaomba tu wananchi wa Iringa mlipe kodi ya majengo na ushuru wa Masniuspaa kwa hiyari kwa kiwango mtakachoelezwa na wataalamu wetu,hii itatusaidia kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwamo afya,miundombinu na elimu”alisema Kimbe.
Awali baraza hilo la  madiwani lilipkea taarifa za utekeelzaji wa miradi yamaendeleo kwa kipindi cha miezi mitatu ya robo ya tatu ya mwaka na kusisitiz aumuhimu w awatendaji kuongez kasi ya utekelezaji wa miradi hiyo.
Diwani wa kata ya Mivinjeni Frank Nyalusi alisema ni muhhimu kwa watednaji kuhakiksha miradi mbalimbali yamaendeleo inatekelezwa kwa wakati ili wananchi waweze kunufaika nayo.
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard  Kasesela alishauri madiwani hao kubuni njia mpya ya  kukusanya mapato zisizo waumiza wananchi.
Kasesela alitoa mfano wa uboreshaji wa gereji bubu na vituo vya kuoshea magari akidai maeneo hayo yanawea kusaidia kuongheza mapato na hata kujenga kituo cha ukaguzi wa magari ambacho kingetumika pia kuongeza kipato.
Katika kikoa hicho Kasesela amesitiza suala mipango miji endelevu yenye kufikiria mbali zaidi, nyumba zote ambazo hazifai kwa makazi wahusika waambiwe ili waweze kuziboresha huku akitaka  Vichoro vyote vilivyo fungwa vifunguliwa ili kuondoa hali hatarishi.

0 maoni:

Chapisha Maoni