Jumanne, 31 Mei 2016

DC KASESELA ATOA ONYO KAL;I KWA WALIMU WANAOFANYA MAPENZI NA WANAFUNZI




 Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akizungumza na wandishi wa habari

Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela awaonya walimu wanaofanya  mapenzi na wanafunzi wao wa kike katika shule mbalimbali za msingi na sekondari wilayani Iringa.

Akizungumza na wanahabari juzi ofisini kwake Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela alisema amepokea taarifa za kusikitisha zinazowahusisha baadhi ya walimu katika shule zilozopo manispaa ya Iringa kufanya mapenzi na watoto ambao ni wanafunzi na kusema kuwa hali  hili inasikitisha.

Kasesela alisema baadhi ya wanafunzi hao wanafanya mapenzi na walimu wao kwa kulazimishwa na kubakwa huku wakipewa vitisho mbalimbali vikiwemo vya kufelishwa mitihani yao.

Alisema Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya hiyo kwa kushirikiana kwa jirani na jeshi la Polisi imeanza kuzifanyia kazi taarifa hizo.

Alisema walimu watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo watachukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria kwa mujibu wa sheria za utumishi na nchi.

“Tayari tumeanza kazi ya uchunguzi wa taarifa hizo katika shule tatu kati yake mbili za mjini na mmoja ipo Iringa Vijijini,” alisema bila kuzitaja shule hizo ili kutovuruga ushahidi.

Alitoa wito kwa wanafunzi wanaolazimishwa na walimu hao kufanyiwa vitendo hivyo kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za siri katika ofisi yake au Polisi.

“Huu ni udhalilishaji mkubwa, hatuwezi kuwavumilia walimu wenye tabia kama hizo na tutajitahidi kupata taarifa zao na kuwachukulia hatua ili kutoa fundisho kwa wengine,” alisema.

 Aliwataka wazazi na walezi wa wanafunzi kuzingatia jukumu lao la malezi bora kwa watoto wao ili kuwaepusha na vishawishi vinavyowza kuwaingiza katika matukio yanayoweza kuwaharibu kitaaluma na kimaisha.

0 maoni:

Chapisha Maoni