Wakala
wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi (NHBRA)
wameanza utafiti wa awali juu kiasi cha nishati kinachotumika katika
shughuli za ujenzi pamoja na michakato yote ya kuandaa vifaa hivyo
ikiemo utengenezaji, uchimbaji, usafirishaji ambapo utaafiti huo una
lengo la kupunguza kiwango cha hewa ya ukaa (greenhouse gases)
kinachotolewa kwenye shughuli za ujenzi hivyo kupunguza uharibifu wa
mazingira.
Wakizungumza
mbele ya wanahabari, Mkandarasi wa NHBRA, Muhandisi Benedict Chilla
ameeleza kuwa kuwa wameweza kufikia mikoa minne na vijiji kadhaa katika
mikoa hiyo ambapo wamebaini mambo mbalimbali wanayoendelea kuyafanyia
utafiti ambapo miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na hewa ukaa ambayo ni
hatari.
“Katika
utafiti huu ambao ni awali tumetumia mwaka mmoja na miezi mitatu.
Miongoni mwa mikoa tuliyoifikia ni pamoja na Tanga, Morogoro, Dodoma na
Dar es Salaam yenyewe ambayo ndio kituo. Tunaamini utafiti huu utaweza
kusanifu majengo yatakayotumia nishati kidogo kwenye hatua ya ujenzi
wake na hata wakati wa matumizi ya majengo husika” alieleza Mhandisi
Benedict Chilla.
Kwa
upande wake, Mhandisi Heri Hatibu amebainisha kuwa, katika utafiti huo
wanatumia mambo mbalimbali ya kitaalamu ambayo yanahitaji uwelewa wa
hali ya juu kuyabaini ikiwemo kukokotoa kiasi cha vifaa vinavyotumika
kwenye ujenzi wa nyumba.
Aidha,
HHBRA wameeleza kuwa, utafit huo umefanyika kwenye maeneo kadhaa
ikiwemo vifaa vya kujengea kuta,(Matofali ya kuchoma, matofali ya
mchanga saruji, matofali ya udongo saruji ya kufungamana.
Pia
vifaa vya ujenzi wa dari (slab) kwa nyumba yenye ghorofa moja na
kuendelea ambapo utafiti wake bado unadelea (dari la zege na nondo,
‘Laad’s, pamoja na ‘waffle’.
Hata
hivyo wataalamu hao wamebaini kuwa matofali ya kuchoma yamekuwa
yakichangia hewa ukaa nyingi kutokana na maandalizi yake ambapo pia ni
miongoni mwa vifaa vya ujenzi vinavyochangia uharibifu wa mazingira kwa
wakati wa maandalizi kwa kutumia kuni nyingi ilikuyachoma
Mkandarasi
wa NHBRA, Muhandisi Benedict Chilla akifafanua jambo katika mkutano
huo kwa wanahabari ( Hawapo pichani) mapema leo jijini Dar es Salaam.
anayemfuatia ni Kaimu Mkuu wa kitengo cha Habari na Masoko wa NHBRA, Bi.
Zubeda Salum
Mkandarasi
wa NHBRA, Mhandisi Heri Hatibu akifafanua jambo namna utafiti huo (Kwa
wanahabari hawapo pichani) utakavyoweza kusaidia Taifa katika masuala
ya ujenzi na kuzuia gesi ukaa. Anayemfuatia ni Kaimu Mkuu wa kitengo cha
Habari na Masoko wa NHBRA, Bi. Zubeda Salum
Kaimu
Mkuu wa kitengo cha Habari na Masoko wa NHBRA, Bi. Zubeda Salum
akifafanua jambo katika mkutano huo. kulia kwake ni Mkandarasi wa
NHBRA, Muhandisi Benedict Chilla na kushoto ni Mkandarasi wa NHBRA,
Mhandisi Heri Hatibu. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog
0 maoni:
Chapisha Maoni