Kaimu
Mkuu wa Mkoa wa Singida na Mkuu wa Wilaya ya Singida, Said Amanzi,
amewataka wananchi kuacha chuki na migogoro isiyokuwa na tija dhidi ya
wawekezaji mbali mbali,kwa madai mambo hayo yanarudisha nyuma maendeleo
ya wilaya na mkoa kwa ujumla.
Amanzi
ametoa wito huo wakati akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa jengo
la kitega uchumi la Blue Plaza lenye ghorofa nne lillilo gharimu zaidi
ya shilingi 1.3 bilioni lililopo mtaa wa highway kata ya Majengo mjini
hapa.
Alisema kwa ujumla uwekezaji una faida nyingi ikiwemo ya kutoa ajira kwa vijana na watu wanaozunguka uwekezaji huo.
Alisema
pamoja na faida lukuki za uwekezaji,bado wapo baadhi ya wakazi wenye
chembechembe ya umwinyi ambao wakiona mwekezaji anapewa eneo la ardhi,
hujitokeza na kuanza kudai eneo hilo ni la babu yake hata kama eneo
husika lipo porini.
“Kumbukumbu
zinaonyesha kuna wakati hospitali kubwa ya St. Gasper inayomilikiwa na
kanisa la Roma Katoliki ilitarajiwa ijengwe katika kijiji cha Kisaki
manispaa ya Singida. Lakini baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Kisaki
wakazua mgogoro ambao ulisababisha hospitali hiyo kujengwa Itigi. Sasa
hivi wakazi hao hao, wanafuata huduma za afya St. Gasper Itigi ambayo
ipo umbali mrefu”,alifafanua.
Akifafanua
zaidi, Amazni alisema wawekezaji wanapaswa kuungwa mkono na kusaidiwa
na wananchi wanaozunguka eneo la uwekezaji, ili wilaya na mkoa uweze
kupiga hatua zaidi katika kujiletea maendeleo endelevu.
Katika
hatua nyingine, DC huyo alisema mmiliki wa jengo la Blue Plaza bwana
Ponsian Rweyemela, ameonyesha njia kwa kuwekeza kwenye ujenzi wa jengo
hili la kitenga uchumi ambalo litatoa ajira, litapendezesha mji wa
Singida na litaongeza mzunguko wa fedha.
“Kwa
ujumla Blue Plaza ni mali ya wakazi wa manispaa ya Singida na
Watanzania wengine watapata fursa ya kufanya shughuli zao zikiwemo za
biashara na kujiingizia kipato, wapo watakaoanzisha ofisi zao humu na
pia manispaa itapata ushuru/ kodi wa kutosha utakaolipwa na jengo hili.
Na Nathaniel Limu
Mmiliki
wa jengo la kitenga uchumi la Blue Plaza la mtaa wa Highway kata ya
Majengo mjini hapa,Ponsian Rweyemela,akitoa nasaha zake kwenye ufunguzi
wa jengo hilo lililo mgharimu zaidi ya shilingi 1.3 bilioni.
Mkuu
wa wilaya ya Singida,Saidi Amanzi akizungumza kwenye hafla iliyofana ya
uzinduzi wa jengo la kitega uchumi la Blue Plaza la mjini hapa.Pamoja
na mambo mengine,DC huyo aliwataka wakazi kuacha chuki na migogoro isiyo
na tija dhidi ya wawekezaji,kwa madai kwamba vitendo hivyo vinarudisha
nyuma maendeleo.
Mkuu
wa wilaya ya Singida,Saidi Amanzi,akikata utepe kuashiria kuzinduliwa
kwa jengo la kitenga uchumi la Blue Plaza mjini hapa.Jengo hilo
lililopendezesha mji wa Singida,litatumika kwa wafanyabiashara,ukumbi za
mikutano na ofisi kwa taasisi mbalimbali
Naibu
mstahiki meya manispaa ya Singida na diwani kata ya Majengo Yagi
Kiaratu,akizungumza kwenye hafla ya chakula cha jioni ikiwa ni sehemu ya
sherehe za uzinduzi wa jengo la Blue Plaza.
Mke
wa mmiliki wa jengo la Blue Plaza,mrs Rweyemela,akitoa shukrani zake
kwa wadau waliojitokeza kuhudhuria uzinduzi wa jengo la Kitenga uchumi
Blue Plaza.
Jengo la kitenga uchumi la Blue Plaza lililo zinduliwa juzi na mkuu wa wilaya ya Singida,Saidi Amanzi.Picha na Nathanile Limu.
0 maoni:
Chapisha Maoni