Jumatano, 1 Juni 2016

Mkoa wa Singida wafungua kitega uchumi kipya, Ni jengo la Blue Plaza kuongeza kasi ya ajira


Kaimu  Mkuu wa Mkoa wa Singida na Mkuu wa Wilaya ya Singida, Said Amanzi, amewataka wananchi kuacha chuki na migogoro isiyokuwa na tija dhidi ya wawekezaji mbali mbali,kwa madai mambo hayo yanarudisha nyuma maendeleo ya wilaya na mkoa kwa ujumla.
Amanzi ametoa wito huo  wakati akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa jengo la kitega uchumi la Blue Plaza lenye ghorofa nne lillilo gharimu zaidi ya shilingi 1.3 bilioni lililopo mtaa wa highway kata ya Majengo mjini hapa.
Alisema kwa ujumla uwekezaji una faida nyingi ikiwemo ya kutoa ajira kwa vijana na watu wanaozunguka uwekezaji huo.
Alisema pamoja na faida lukuki za uwekezaji,bado wapo baadhi ya wakazi wenye chembechembe ya umwinyi ambao wakiona mwekezaji anapewa eneo la ardhi, hujitokeza na kuanza kudai eneo hilo ni la babu yake hata kama eneo husika lipo porini.
“Kumbukumbu zinaonyesha kuna wakati hospitali kubwa ya St. Gasper inayomilikiwa na kanisa la Roma Katoliki  ilitarajiwa ijengwe katika kijiji cha Kisaki manispaa ya Singida. Lakini baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Kisaki wakazua mgogoro ambao ulisababisha hospitali hiyo kujengwa Itigi. Sasa hivi wakazi hao hao, wanafuata huduma za afya St. Gasper Itigi ambayo ipo umbali mrefu”,alifafanua.
Akifafanua zaidi, Amazni alisema wawekezaji wanapaswa kuungwa mkono na kusaidiwa na wananchi wanaozunguka eneo la uwekezaji, ili wilaya na mkoa uweze kupiga hatua zaidi katika kujiletea maendeleo endelevu.
Katika hatua nyingine, DC huyo alisema mmiliki wa jengo la Blue Plaza bwana Ponsian Rweyemela, ameonyesha njia kwa kuwekeza kwenye ujenzi wa jengo hili la kitenga uchumi ambalo litatoa ajira, litapendezesha mji wa Singida na litaongeza mzunguko wa fedha.
“Kwa ujumla Blue Plaza ni mali  ya wakazi wa manispaa ya Singida na Watanzania wengine watapata fursa ya kufanya shughuli zao zikiwemo za biashara na kujiingizia kipato, wapo watakaoanzisha ofisi zao humu na pia manispaa itapata ushuru/ kodi wa kutosha utakaolipwa na  jengo hili.
Na Nathaniel Limu
IMG_5600Mmiliki wa jengo la kitenga uchumi la Blue Plaza la mtaa wa Highway kata ya Majengo mjini hapa,Ponsian Rweyemela,akitoa nasaha zake  kwenye ufunguzi wa jengo hilo lililo mgharimu zaidi ya shilingi 1.3 bilioni.
IMG_5603Mkuu wa wilaya ya Singida,Saidi Amanzi akizungumza kwenye hafla iliyofana ya uzinduzi wa jengo la kitega uchumi la Blue Plaza la mjini hapa.Pamoja na mambo mengine,DC huyo aliwataka wakazi kuacha chuki na migogoro isiyo na tija dhidi ya wawekezaji,kwa madai kwamba vitendo hivyo vinarudisha nyuma maendeleo.
IMG_5606Mkuu wa wilaya ya Singida,Saidi Amanzi,akikata utepe kuashiria kuzinduliwa kwa jengo la kitenga uchumi la Blue Plaza mjini hapa.Jengo hilo lililopendezesha mji wa Singida,litatumika kwa wafanyabiashara,ukumbi za mikutano  na ofisi kwa taasisi mbalimbali
IMG_5673Naibu mstahiki meya manispaa ya Singida na diwani kata ya Majengo Yagi Kiaratu,akizungumza kwenye hafla ya chakula cha jioni ikiwa ni sehemu ya sherehe za uzinduzi wa jengo la Blue Plaza.
IMG_5723Mke wa mmiliki wa jengo la Blue Plaza,mrs Rweyemela,akitoa shukrani zake kwa wadau waliojitokeza kuhudhuria uzinduzi wa jengo la Kitenga uchumi Blue Plaza.
IMG_5494Jengo la kitenga uchumi la Blue Plaza lililo zinduliwa juzi na mkuu wa wilaya ya Singida,Saidi Amanzi.Picha na Nathanile Limu.

0 maoni:

Chapisha Maoni