Jumatano, 1 Juni 2016

TABIA HATARI YA VIRUSI VYA UKIMWI

VIRUSI VYA UKIMWI vina ngazi zake katika mwili wabinadamu. moja yan tabia au ngazi ni kujigeuza geuza.

Virusi hivyo katika tabia yake ya Nne, vinajigeuzageuza na kutokuwa kiumbe hai kwa wakati (They can stay in dormany stage) yaani kama inavyokuwa mbegu za mazao.
Virusi hivi vinashambulia kinga za mwili ambapo utendaji wa kinga za mwili ni sawa na ulinzi wa nchi ingawa tofauti yake kubwa ni kwamba nchi tayari askari wapo lakini mwili unaanza kutengeneza askari pale adui anapoingia na kisha hutuma mashushushu.
Askari wa mwili wanaitwa Antibodies na adui anaitwa antigen ambapo VVU humla askari anayetumwa kufanya ushushushu waitwao CD4, hivyo taarifa sahihi hazipatikani katika chuo cha kutengeneza askari na akitokea shushushu mmoja ametoroka bila kuliwa, hupeleka taarifa ambazo haziwezi kufikia malengo ya kukabiliana na adui.
Kipindi hiki kidaktari huita kipindi cha mpito yaani kipindi cha dirisha la mpito (Window period). Kipindi hiki mtu anaonekana mzima na hata akipimwa VVU havionekani.

0 maoni:

Chapisha Maoni