Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe
13 Juni, 2016 amewaapisha mawaziri wawili kufuatia mabadiliko madogo ya
Baraza la Mawaziri aliyoyafanya Jumamosi tarehe 11 Juni, 2016.
Mawaziri
walioapishwa leo Ikulu Jijini Dar es salaam ni Mhe. Mwigulu Lameck
Nchemba aliyeapishwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mhe.
Mwigulu Lameck Nchemba ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi
anakwenda Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, akitokea Wizara ya Kilimo,
Mifugo na Uvuvi.
Waziri mwingine ni Dkt. Charles John Tizeba ambaye ameapishwa kuwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
Dkt.
Charles John Tizeba ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Buchosa aliteuliwa na
Rais Magufuli kuwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi kuanzia tarehe 11
Juni, 2016.
Hafla ya kuapishwa kwa Mawaziri hao imehudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.
Imetolewa na :
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU Dar es salaam, Gerson Msigwa
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli,
akimuapisha Mh. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
leo Ikulu Jijini Dar es Salaam
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akimkabidhi hati
ya kiapo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mwigulu Nchemba mara
baada ya kumuapisha leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli
akimuapisha Dkt. Charles Tizeba kuwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi
leo Ikulu Jijini Dar es Salaam
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akisaini hati ya
kiapo mara baada ya kumuapisha Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Dkt.
Charles Tizeba Leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Tizeba na Waziri wa Mambo ya
Ndani ya Nchi Mh. Mwigulu Nchemba wakipongezana mara baada ya kuapishwa
Leo Ikulu Jijini Dar es Salaam
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akimpongeza
Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Tizeba mara baada ya
kumuapisha Leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Mambo ya
Ndani ya Nchi Mh. Mwigulu Nchemba
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli akiwa katika
picha ya pamoja na Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Tizeba
(kulia) na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Mwigulu Nchemba mara
baada ya kuwaapisha Leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.PICHA NA HASSAN
SILAYO-MAELEZO
0 maoni:
Chapisha Maoni