Wakala wa Barabara nchini TANROADS Mkoa wa Dar es Salaam  kupitia mpango wao w akupunguza foleni katika jiji la Dar es Salaam, wamejidhatiti kuakikisha wanapunguza msongano wa foleni kwa kuendelea kukarabati barabara za pembezoni na zile za katikati kwa kiwango cha lami ilikuondokana na foleni kwa sasa.
Akizungumza na waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam leo Juni 13.2016, Mhandisi wa miradi na madaraja wa TANROADS, Bwana Ngusa Julius amesema tayari karibu maeneo yote ya baranara hizo taraibu zinaendelea huku maeneo mengine zikiwa hatua ya mwisho na barabara zingine zikiwa tayari zimekamilika na zinatumiwa kwa kiwango kikubwa kwa sasa.
Mhandisi huyo amebainisha kuwa,  foleni nyingi zinazoikumba jiji la Dar es Salaam ni kutokana na madereva wengi kukumbia barabara za vumbi hivyo wengi kujikuta wanatumia barabara za lami kwa kiwango kikubwa.
“Katika jiji la Dar es Salaam barabara nyingi za mitaa ni za vumbi, na zina mashimo makubwa ambayo yanasababisha magari kushindwa kupita. Kutokana na hali hii madereva wa magari wanapendelea kutumia barabara za lami zilizopo hata wanapotaka kwenda maeneo ya jirani na alipo hivyo kuwepo na msongamano mkubwa sana kwenye barabara hizo kwa sababu kunakuwepo kwa mwingiliano mwingi sana wa magari wakati wa kuingia na kutoka kwenye barabara ya lami.
Ili kupunguza msongamano wa aina hiyo, Wizara ilibuni mradi wa barabara kupunguza msongamano katika jiji la Dar es Salaam na Wakala wa Barabara nchini ilianza kutekeleza mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami” alieleza Mhandisi  Ngusa Julius.
Aidha alizitaja barabara ambazo zimeainishwa kwenye mpango huo wa ujenzi wa barabara kuwa ni pamoja na:- Ubungo bus terminal – Kigogo – Kawawa road roundabout – (km 6.4). Kigogo Round about – Jangwani – Twiga (km 2.72), Tabata Dampo – Kigogo na Ubungo Maziwa Mabibo External (Mandela) km 2.25.
Pia zipo barabara za Jet Corner – Vituka – Davis Corner – (km 12), Mbezi – Malambamawili – Kinyerezi – Banana – (km 14), Old Bagamoyo na TPDC (Garden) km 9.1, Tegeta Kibaoni – Wazo Hill – Goba – Mbezi/Morogoro Road – (km 18).
Tanki bovu – Goba (km 9.0), Kimara Baruti – Msewe – Changanyikeni (km 2.6), Kimara – Kilungule – External (Mabibo Mandela) km 9.0, Bunju B Mpiji Magohe Victoria Kifulu hadi Pugu Kiltex 33.7 (Outer ringroad) na Banana – Kinyerezi – Kifuru – (km 8)
Mhandisi Ngusa Julius amebainisha kuwa, katika awamu za fedha baadhi ya miradi ilianza na mingine kukamilika ikiwemo madaraja ili kusaidia kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam.
Aidha amebainisha kuwa, Kuchelewa kukamilika kwa mradi huu ulitokana na wanachi wa eneo la Mchikichini kugoma kubomoa nyumba zao licha ya kulipwa fidia kwa kufungua kesi mahakamani ya madai ya kuongezewa fidia.
“Sababu ni nyingi ikiwemo kuchelewesha malipo ya mkandarasi kumechangia kumaliza kazi za ujenzi mapema. Kwa sasa mkandarasi anakamilisha kazi za ujenzi baada ya kulipwa sehemu ya madai yake zitakamilika ifikapo mwisho mwa mwezi Juni 2016.” Alieleza Mhandisi huyo.
Kwa upande wake Afisa Habari wa TANROADS, Bi. Aisha Malima ametoa rai kwa wananchi kuendelea kuzitunza barabara hizo kwani zinagharimu fedha nyingi katika ujenzi wake na pia katika utunzaji wake hivyo wananchi wametakiwa kuchukua hatua za kuzirinda.
DSC_7599Maafisa wa TANROADS wakiwa katika mkutano huo na waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam kuelezea namna ya kupunguza msongamano wa foleni
DSC_7603Mhandisi wa miradi na madaraja wa TANROADS, Bwana Ngusa Julius akielezea namna walivyoweza kujenga barabara  kwa kiwango cha lami katika jiji la Dar es Salaam sambamba na madaraja yanayounganisha barabara hizo.
DSC_7592Mhandisi wa miradi na madaraja wa TANROADS, Bwana Ngusa Julius (kushoto) akifafanua jambo, kulia kwake ni Afisa Habari wa TANROADS, Bi. Aisha Malima. (Picha zote na Andrew Chale]