Serikali
kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto
inaendelea na utaratibu wa kutoa taarifa ya mwenendo wa mlipuko wa
ugonjwa Kipindupindu nchini kila wiki kama tulivyoahidi, ili kutoa
tahadhari kwa wananchi na maelekezo ya hatua za kuchukua ili kukabiliana
na mlipuko huu.
Hadi kufikia tarehe 12 Juni 2016, jumla ya wagonjwa 21,786 nchini
wametolewa taarifa,na kati yao Ndugu zetu 342 wamepoteza maisha tangu
ugonjwa huu uliporipotiwa Agosti 2015.
Takwimu
zinaonyesha kuwa, katika wiki hii inayoishia tarehe 12 Juni 2016,
Idadi ya wagonjwa walioripotiwa nchi nzima ni 78 na kati yao mmoja
alipoteza maisha. Wiki iliyotangulia kulikuwa na wagomjwa 62
waliotolewa taarifa na kati yao watatu walipoteza maisha. Hii ikionyesha
kuna ongezeko la wagonjwa walioripotiwa wiki hii ikilinganishwa na wiki
iliyotangulia ingawa kuna kupungua
Takwimu
zinaonyesha kuwa, katika wiki hii inayoishia tarehe 12 Juni 2016,
Idadi ya wagonjwa walioripotiwa nchi nzima ni 78 na kati yao mmoja
alipoteza maisha. Wiki iliyotangulia kulikuwa na wagomjwa 62
waliotolewa taarifa na kati yao watatu walipoteza maisha. Hii ikionyesha
kuna ongezeko la wagonjwa walioripotiwa wiki hii ikilinganishwa na wiki
iliyotangulia ingawa kuna kupungua
kwa Idadi ya waliopoteza maisha.
Mikoa
iliyoripoti ugonjwa wa kipindupindu wiki hii ni mitano(5), Morogoro (
wagonjwa 43 na kifo 1), Mwanza (21), Mara (7), Lindi (4) na Manyara
(3). Aidha wiki hii wilaya zilizoripoti ugonjwa wa Kipindupindu ni
Morogoro vijijini (wagonjwa 27 na kifo 1), Morogoro mjini (8), Mvomero
(8), Ilemela (12), Nyamagana (9), Tarime vijijini (5), Tarime mjini (2),
Kilwa (4) na Simanjiro (3). Mpaka sasa bado mikoa ya Njombe na
Ruvuma haijaripoti mgonjwa yeyote wa Kipndupindu tangu mlipuko huu
uanze mnamo mwezi Agosti mwaka 2015
Licha
ya kuwa kwa ujumla kasi ya mwenendo wa ugonjwa wa kipindupindu imekuwa
ikipungua, takwimu hizi zinaashiria kuwa ugonjwa wa kipindupindu bado
upo katika jamii tunazoishi na unagharimu maisha ya watu ambao ni nguvu
kazi ya Taifa.
Hivyo
wote kwa pamoja hatuna budi kuendeleza juhudi za ufuatiliaji na
mapambano dhidi ya ugonjwa huu na tuendelee kutekeleza na kusimamia
kikamilifu maelekezo na miongozo stahili inayotolewa na Wizara yangu.
Wizara
yangu inaendelea kutoa onyo kali kwa Wasimamizi wa huduma za Afya
Mikoani na katika Halmashauri, ambao wanaficha taarifa za wagonjwa wa
Kipindupindu. Yeyote atakayebainika kuwa anaficha taarifa hizi
atachukuliwa hatua kali. Wizara yangu inasisitiza kuwa, juhudi za
kusimamia kikamilifu hatua mbalimbali za udhibiti wa mlipuko huu
ziendelee.
Aidha
katika kipindi hiki ambapo ugonjwa unaendelea kupungua,Wasimamizi wa
huduma za Afya Mikoani na katika Halmashauri, waendelee kufuatilia na
kuchunguza kwa kina, taarifa zote za vifo vinavyotokana na mgonjwa
mwenye dalili za Kipindupindu kama kuharisha na kutapika. Taarifa hizi
zinahitajika ili hatua madhubuti za kuzuia vifo ziweze kuchukuliwa.
Wizara
inaendelea kuwapongeza na kuwashukuru wadau wote kwa jitihada za dhati
zinazoendelea kutekelezwa na katika kusimamia kikamilifu miongozo
inayotolewa na Wizara ili kuutokomeza ugonjwa huu, ikiwa ni pamoja na
wataalamu wa sekta mbalimbali, Mashirika ya Kimataifa, Watumishi, Mikoa
na Halmashauri pamoja na waandishi wa habari na wananchi kwa ujumla.
0 maoni:
Chapisha Maoni