Baada
ya mwezi Januari mcheza wa tenesi, Maria Sharapova vipimo kuonyesha
kuwa anatumia dawa za kuongeza nguvu mwilini, hatimaye hukumu yake
imetolewa na Shirikisho la Kimataifa la Tenesi kwa kumfungua miaka
miwili asicheze tenesi.
Sharapova
aligundulika kutumia madawa hayo wakati alipofanyiwa vipo katika
mashindano ya Australia Open na baada ya kugundulika kutumia dawa hizo
alizuiliwa kushiriki mashindano hayo na kusubiri hatua ambazo
zingekufuatia ambapo sasa ndiyo hukumu imetolewa.
Hata
hivyo taarifa zinaeleza kuwa Sharapova amepanga kwenda katika mahakama
ya michezo kwa ajili ya kukata rufaa ya adhabu hiyo ambayo imetolewa
kwake kwa kutumia madawa ya kuongeza nguvu ya meldonium.
Wakati
hayo yakimkuta, kampuni ya vifaa vya michezo ya Nike ambayo inafanya
kazi na Sharapova imetoa taarifa kuwa itaendelea kufanya kazi na
Sharapova na wanaamini ataenda mahakamani kukata rufaa ili arejee
michezoni.
0 maoni:
Chapisha Maoni