Zikiwa
zimebakia siku chache kuondoa simu feki Tanzania; huku zoezi hili
likitazamiwa kuathiri mamilioni ya watumiaji wa simu za mikononi nchini
kote, kampuni nguli ya utengenezaji wa simu za mkononi kutoka China,
Huawei imeendelea kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha upatikanaji wa
simu zilizo bora kwa Watanzania.
Katika
kufanikisha adhma hii ya kuondoa simu zote zisizokidhi ubora
zilizofurika sokoni na kuhakikisha watanzania wana uwanja mpana wa
kupata simu bora za mkononi, Huawei Tanzania hivi karibuni wamezindua
aina mbalimbali za simu za mkononi ili kukidhi mahitaji ya wateja wao
kiuchumi na hali tofauti za maisha.
Simu
hizo ni kama GR5,Y6 Pro,Y6 Pro 4G ,Mate 8 32GB,Mate 8 64GB,Y3 lite,Y3
II,GR3,Y6, Y5C,Y3C,Shot X, Mate S, P8 64GB,P8 32GB,G8, P8 lite ,G play
min,P9, na P9 lite. Kwakua soko la Tanzania ni pana na lina utofauti
Huawei Tanzania wamejikita katika kuboresha vifaa vyao kwa kutenga
asilimia kumi ya mapato yao katika kuwekeza kwenye soko ili kuongeza na
kuboresha vifaa na simu za kisasa za Huawei. Huawei imeazimia kuwa
kinara katika soko na kilele cha ubora.
Moja ya simu ambayo Huawei wameizindua, P9 Lite
Watanzania
pia wamesisitizwa kuhakiki simu zao kabla ya katika ya mwezi Juni. Rai
hii imetolewa na Bwana Hu Xiangyang Jacko, Meneja wa Huawei nchini
Tanzania, akizingatia kuwa watanzania wengi hawana elimu na uelewa wa
kutosha wa namna ya kuhakiki simu zao.
“Ni
muhimu sana kuhakiki simu yako unapoinunua ili kuwa na uhakika kuwa
simu hiyo ni orijino. Ili mteja afahamu kuwa simu yake ni halisi au la,
apige *#06# kwenye simu yeyote, atapata IMEI namba kisha atume namba
hizo kwenda 15090 ili kupata ujumbe kama simu hiyo ni halisi ama la. Kwa
simu za Huawei mteja atapokea ujumbe kutoka TCRA ukiwa na aina ya simu
mfano (Huawei Technologies Co Ltd-Huawei Mate 8)”. Alisema Bwana Jacko.
Kwa
mujibu wa TCRA takribani asilimia 40 ya simu za mkononi zinazotumiwa na
watanzania ni feki. Simu feki sio tishio tu kwa wauzaji wa simu za
mkononi bali pia kwa serikali na taifa kwa ujumla. Wakati Mamlaka ya
Mawasiliano (TCRA) imeazimia kuzima simu zote feki nchi nzima, Huawei
Tanzania wanaona mpango huu upo sawia na mikakati yake katika
kukabiliana na uhalifu, kuongeza mapato, kuwalinda wateja na simu zilizo
chini ya viwango, kulinda matumizi ya fedha kupitia simu au miamala
inayofanywa kwa njia ya simu pamoja na kuruhusu mawasiliano yaliyo bora
nchini kote.
Kuna
upotoshaji ulioshika kasi nchini Tanzania kuwa simu yoyote iliyo na
kioo cha kugusa “touch screen” ni smartphone. Na hii ndio iliyopelekea
kuongezeka kwa idadi ya simu feki katika soko la Tanzania. Kifupi
smartphone inamuwezesha mtumiaji kupiga simu, ina sifa kama za kompyuta
au laptop, uwezo wa kupata huduma za intaneti na kadhalika.
Pia
tofauti na mawazo ya wengi kuwa bidhaa zote kutoka China ni feki au ni
za kiwango cha chini katika ubora, Huawei kama bidhaa ya kimataifa
imeendelea kuthibitisha msimamo wake kutengeneza bidhaa zilizo bora kwa
wateja wake katika masoko yao yote.
Akielezea
hilo Bwana Sylvester Manyara Mkurugenzi wa Mauzo ya Rejareja, Huawei
Tanzania anasema “Huawei inaongoza katika kutoa masuluhisho ya
teknolojia na habari duniani, kampuni hii ilipokea zawadi ya ubora
China, zawadi ya kiheshima kwa ubora wa bidhaa China, Machi 29. Huawei
ilipata zawadi ya juu katika watengenezaji katika kitengo cha wateja na
msimamo wa ubora.
Aidha
Kansela Yong Wang alitoa zawadi hiyo kwa Huawei katika ukumbi wa Great
Hall jijini Beijing Machi 29 2016. Hiyo ni zawadi kubwa katika serikali
ya China kwa ajili ya bidhaa zilizo na ubora. Bidhaa zilizo na ubora wa
kipekee na watu wanaoonyesha mafanikio ya kipekee ndio wanaopewa zawadi
hiyo.”
Akizungumzia
ubora wa vifaa vya Huawei, Bwana Hu Xiangyang Jacko, Meneja Mkazi wa
Huawei Tanzania alisema “Huawei tunaamini kuwa ubora ndio fahari yetu.
Zawadi ya ubora China ni alama ya msimamo endelevu wa Huawei katika
ushindi. Kwa takribani miaka ishirini, Huawei kama Kampuni iliyojikita
kutimiza mahitaji ya wateja imeweka mkazo katika uvumbuzi na ubora wa
bidhaa. Huawei itaendelea kufanya Juhudi katika ubora na kutengeneza
bidhaa zilizobora kwa wateja wetu duniani na Tanzania.”
Mahitaji
ya wateja yamekua kiangalizo kikubwa katika shughuli za Huawei. Toka
mwaka 1987, Huawei imeweka wateja wake karibu na inalenga kutengeneza
bidhaa za ubora wa hali ya juu kwa namna ya pekee. Miaka ishirini na
nane baadae, Huawei imezawadiwa kote China na nchi za nje kwa ubora wa
viwango. Bidhaa za Huawei sasa zinapatikana zaidi ya nchi 170 na
asilimia sitini ya mapato ya Kampuni yanatoka katika masoko ya nje.
Huawei
imeweka mpango madhubuti wa huduma kwa mteja, unao wawezesha kupata
maoni yote ya wateja wao kupitia namba ya simu, mitandao na maoni haya
hutumika katika uvumbuzi na maendeleoa ya bidhaa. Katika safari yao ya
ubora, mwaka 2014 Huawei ilishika nafasi ya 94 kwenye Interbrand Top 100
ya Kampuni zinazothaminiwa duniani, ikiwa Kampuni ya kwanza kutoka
China kuingingia katika orodha hiyo. Mwaka mmoja baadae, Huawei imepata
mafanikio Zaidi na kushika nafasi ya 88.
Kiujumla,
katika ripoti za hivi karibuni imeshika nafsi ya 47 na ikiwa na thamani
ya dola bilioni 19.7. Hii imefanya Huawei kuwa kampuni ya kwanza ya
kichina kuingia katika 50 bora. Kampuni ya Huawei pia imetambuliwa na
shirika la Kimarekani US-based Reputation Institute kama Kampuni pekee
ya kichina kuwa katika kumi bora ya Kampuni zinazoheshimika China.
Pamoja
na ushirikiano kutoka TCRA, wadau wake na wateja wake, Huawei Tanzania
imekua kwa kasi kubwa toka ilipoingia katika soko la Tanzania. Na
msimamo wao wa ubora na kukidhi mahitaji ya wateja wao, Huawei
itaendelea kudumu. Kupitia kampeni ya TCRA kuondoa simu zote feki na
matatizo yanayohusiana na simu hizo, Huawei inaamini kuwa itakua bidhaa
pendwa ya Tanzania.
Tanzania
ni miongoni mwa nchi za Afrika ikiwemo Kenya, Uganda na Zambia ambazo
zimechukua hatua kuzima simu zenye IMEI namba feki. Huawei ikiwa kampuni
inayoongoza kwa simu za mkononi Tanzania inawaahidi Watanzania wote
kupata na kufurahia simu zilizohalisi na kwa bei nafuu. Kampuni ya
Huawei imetoa ahadi kuongeza ubora wa bidhaa kwa asilimia 30 kila mwaka.
0 maoni:
Chapisha Maoni