Uhusiano
kati ya Marekani na Tanzania unaonesha dalili za kuimarika licha ya nchi
hiyo kukatiza msaada wa awamu ya pili ya mradi wa changamoto za milenia
(MCC-2) kwa Tanzania.
Balozi wa
Marekani nchini Tanzania Mheshimiwa Mark Childress amesema hayo baada
ya kukutana na kufanya mazungumzo na rais wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli.
Bwana
Childress alisema kuwa hivi karibuni ''kupitia shirika la misaada la
Marekani, USAID tunatarajia kutia saini mkataba wa zaidi ya dola milioni
400 kwa ajili ya mwaka ujao.
''Aidha
tumezungumza kuwa kutakuwa na dola milioni 800 zitakazotolewa na
Marekani kwa ajili ya miradi mbalimbali na hii haihusiani na MCC.''
Alisema balozi Childress
"Ukweli
ni kwamba tunayo mengi ya kufanya pamoja katika sekta mbalimbali
zikiwemo afya, elimu na kilimo na tutafanya kila juhudi kuhakikisha
yanafanikiwa"
Rais Magufuli kwa upande wake alisema kuwa serikali yake itaendeleza kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano na Marekani.
0 maoni:
Chapisha Maoni