Jumanne, 7 Juni 2016

WAFUGAJI WADOGO WALIA NA BEI NDOGO YA MAZIWA




Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Ushirika (WKMU) sehemu ya mifugo, Dkt. Maria Mashingo (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa mfugaji wa mdogo wa ng'ombe wa maziwa mjini Njombe Paul Kasunga alipotembelea banda hilo maonesho wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya unywaji wa maziwa yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe wiki iliyopita. (Picha na Friday Simbaya) 




Ng'ombe wa maziwa aina ya Ayshire ambaye ana umri miaka mitano anauwezo wakutoa lita 22 ya maziwa kwa siku. 





Small milk producer Wema Gilbert Ngimbuchi (blind) of Ikuna Village Ikuna in Ward, Njombe district sings before the Permanent Secretary in the Ministry of Agriculture, livestock and Cooperatives (livestock section) Dr. Mary Mashingo (left) as a sign of thankfulness after she was handed over a registration certificate as a milk producer supplied by Tanzania Dairy Board (TDB) during the peak week of drinking milk made nationally in Njombe region last week. The Staff of the East Africa Dairy Development (EADD II) for their unity, they performed an act of mercy by the presenting a cow to her (Wema Ngimbuchi) worth Tsh. 1,000,000/=. (Photo by Friday Simbaya)



Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Ushirika (sehemu ya mifugo) Dkt. Maria Mashingo (kushoto) akipeana mkono na mzalishaji mdogo wa ng'ombe wa maziwa Wema Gilbert Ngimbuchi (mlemavu wa macho) wa Kijiji cha Ikuna Kata ya Ikuna, wilyani Njombe, mkoani Njommbe baada ya kumkabidhi cheti cha usajili cha mzalishaji mdogo wa maziwa kilichotolewa na Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB) wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya unywaji wa maziwa yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe wiki iliyopita. Wafanyakazi wa Mradi wa uendelezaji sekta ya maziwa Afrika Mashariki (EADD II) awamu ya pili kwa umoja wao,walifanya tendo la huruma kwa kumzawadia mfuaji huyo mtamba wa ng`ombe mwenye thamani ya Tsh. 1,000,000/=. (Picha na Friday Simbaya)






Permanent Secretary in the Ministry of Agriculture, livestock and Cooperatives (livestock section) Dr. Mary Mashingo (left) shakes hand with small milk producer Wema Gilbert Ngimbuchi (blind) of Ikuna Village Ikuna in Ward, Njombe district, after handed over a registration certificate as a milk producer supplied by Tanzania Dairy Board (TDB) during the peak week of drinking milk made nationally in Njombe region last week. The Staff of the East Africa Dairy Development (EADD II) for their unity, they performed an act of mercy by the presenting a cow to her (Wema Ngimbuchi)worth Tsh. 1,000,000/=. (Photo by Friday Simbaya) 




Baadhi ya wafanyakazi wa Mradi wa uendelezaji sekta ya maziwa Afrika Mashariki (EADD II) kutoka mikoa ya Mbeya, Njombe na Iringa wakiwa katika picha ya pamoja.




Mfugaji wa ng’ombe wa maziwa kutoka kitovu (dairy hub) kutoka kikundi cha wafugaji wadogo Halmashauri ya Njombe (WAWAHANJO) katika kijiji cha Ikando Rahel Mhema akiongea na mwandishi wa habari nyumbani kwake katika Ikando wilaya Njombe mkoani njombe.










Mfugaji wa ng’ombe wa maziwa kutoka kitovu (dairy hub) kutoka kikundi cha wafugaji wadogo Halmashauri ya Njombe (WAWAHANJO) katika kijiji cha Ikando Rahel Mhema akionesha marobota yako ya hei (majani ya Rhodes boma) katika sehemu kavu iliyoezekwa kuzuia jua na mvua alipotembelewa na mwandishi wa habari hivi karibuni. Mfugaji huyo alipata mafunzo ya dhana ya kutengeneza hei kwa njia rahisi ya kufunga marobota ya hei kwa njia mkono kutoka Mradi wa uendelezaji sekta ya maziwa Afrika Mashariki (EADD II) awamu wa pili kwa kushirikana na Heifer International.
























Mfugaji wa ng’ombe wa maziwa kutoka kikundi cha wafugaji wadogo cha mshikamano Efrahana Kidenya katika kijiji cha Mhaji wilayani Wanging’ombe, Mkoa wa Njombe akiwa katika shamba la ekari moja la malisho la majani (hei) aina ya Rhodes boma. 



Ndama aliyezaliwa kwa njia Uhimilishaji












Bustani ya mboga za majani (kitchen garden).






Mshauri mwandamizi wa biashara kutoka EADD II mkoa wa Njombe Joseph Lyamuya (kulia) akiwa mfugaji kutoka katika kijiji cha Mlevela kata ya Igima wilayani Wanging’ombe, Mkoa wa Njombe.












Mfugaji wa ng’ombe wa maziwa Catherine Mlowe akiwa na mme wake kutoka katika kijiji cha Mlevela kata ya Igima wilayani Wanging’ombe, Mkoa wa Njombe akionesha sehemu ya kuhifadhia mkojo wa ng’ombe kutoka banda la ng'ombe unayotumika kama mbolea kwenye bustani ya mboga za majani (kitchen garden).




Mradi wa uendelezaji sekta ya maziwa afrika mashariki (EADD II) awamu ya pili umeinua kipato cha wafugaji wa ng’ombe wa maziwa katika mikoa ya Njombe, Iringa na Mbeya kwa kuwajengea uwezo wa kutumia fursa ya kukusanya maziwa kwa pamoja, kupata mafunzo na huduma mbalimbali za ufugaji na biashara ya maziwa kupitia vyama vya wafugaji.

Meneja wa mradi nchini Mark Tsoxo aliwaambia mtandao wa KALI YA HABARI jana kuwa mradi huo umeweza kufanya wafugaji wadogo wa ng’ombe wa maziwa kuwa na mahali pakukusanyia na kuhifadhi maziwa kwa wingi (dairy hubs), upatikanaji wa huduma za kinga na tiba ya mifugo, uboreshaji wa koosafu (breeding line) ya ng’ombe, upatikanaji wa mbegu za malisho, vyakula vya ziada vya mifugo pamoja na kutoa ushauri na huduma za ugani.

Tsoxo alisema kuwa EADD II itawawezesha wafugaji kitaalamu kutumia teknolojia mpya na stadi za uzalishaji malisho, kuwa na vyanzo mbadala vya vyakula bora vya mifugo, ukusanyaji, upoozaji na usafirishaji wa maziwa.

Alisema kuwa mradi huu wa EADD II utaweka kupaumbele katika kuuganisha nguvu ya pamoja ya wafugaji na usawa wa kijinsia ili kuongeza tija kuwanufaisha walengwa katika kaya zipato 136,000 katika Afrika Mashairiki na jamii kwa ujumla. Kwa Tanzania mradi umelenga kunufaisha kaya 35,000. 


Mradi huu unatekelezwa na ushirikiano baina ya mashirika matano ya maendeleo. Mashirika hayo ni Heifer International Tanzania (ushauri na huduma za ugani), Technoserve (ushauri wa biashara na masoko), ICRAF (mazingira na malisho), African Breeders Service (Uhimilishaji) na International Livestock Research Institute (Masuala ya utafiti)

0 maoni:

Chapisha Maoni