Alhamisi, 8 Septemba 2016

WALIMU 2000 WAHITIMU MAFUNZO YA KKK WILAYA YA RUNGWE MKOANI MBEYA

Posted by Esta Malibiche on Sept8.2016 in News






NAIBU Waziri wa Tamisemi Suleiman Jaffo amewataka wahitimu wa mafunzo ya uwalimu kuhakikisha wanafanya kazi kwa kuzingatia weredi  wa taaluma yao ili kuleta heshima na ufanisi mkubwa mahali pa kazi.
Kauli hiyo aliitoa juzi wakati akifunga mafunzo ya walimu  wa kkk yaliyofanyika katika chuo cha  ualimu Tukuyu mkoani Mbeya,ikiwa ni moja ya ziara yake aliyoifanya mkoani Mbeya  ambapo zaidi ya walimu 2000 wamepata mafunzo hayo.
Waziri Jaffo katika ziara yake hiyo alizungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Rungwe na kuwataka kufanya kazi kwa bidii ikiwa nipamoja na kudumisha upendo na Amani katika maeneo na kushirikiana na wananchi ili kubaini changamoto zinazowakabili na hatimae serikali iweze kuzitatua
Aidha Jafo alitembelea Hosipitali ya wilaya ya Rungwe Makandala na  kubaini changamoto kadhaa ikiwa nipamoja na  kukosekana kwa kutumia mashine ya kutolea risiti ya EFDs katika Hospital hiyo hali iliyosababisha Naibu waziri kupigwa butwaa.Alifika hospitalini hapo juzi na kwenda moja kwa moja kwenye dirisha la malipo kisha akaomba kuandikishwa na kuomba risiti ndipo alipougundua kua Hospital hiyo haikuwa na mashine za kutolea Risiti na hatimae alipewa lisiti ya kawaida iliyoandikwa na mkono.
Baada ya kupokea risiti hiyo ilimlazimu  kufanya mazungumzo na Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo, Dk. Marco Mbata na mweka hazina  wa Halmashauri hiyo  kujua sababu za kutumia mfumo ambao ulishapigwa marufuku  na serikali na kuagizwa kufunga mfumo wa kieletroniki ili kudhibiti mapato.
 “Kwanza hii risiti yenyewe ni feki….. nilishaagiza ifikapo Julai 30 mwaka huu kila hospitali iwe imefunga mfumo wa kieletroniki, na hospitali zote zilizofunga zimeongeza mara dufu mapato yake  lakini nyinyi bado mnaendelea na mfumo huu ambao mnatumia kuiba fedhaza Serikali. Nimesikitishwa na kitendo hiki cha kuioibia Serikali mapato kwa kwa kutumia  vitabu  vyenu kuandikia risiti za mkono na hatimae mnakwepesha mapato kwa kujiingizia kwenye mifuko yenu,kwa hali hii hatapona mtu,” alisema Jafo.
Naibu Waziri alihoji kiasi kinachokusanywa  kwa mwezi kutokana na kutoa risiti za mkono,ambapo Mbata alisema wanakusanya Sh3 milioni, jambo lililonekana kuibua hasira kwa Naibu Waziri huyo akisema huo ni mpango wa kuendelea kuiba mapato kwa kuendelea risiti za mkono na kutishia kuwatimua kazi Mbata na mweka hazina wa halmashauri kutokana na kuidanganya serikali.
Naibu Waziri, Jafo hakuweza kukubaliana na utetezi huo huku akitoa siku 25 kuanzia jana wawe wamefunga na kuanza kutumia mashine za kieletroniki na  endapo itafika  Septemba 30 mwaka huu hawajafunga mfumo huo basi Mganga Mkuu na Mweka hazina wa halmashauri hiyo watakuwa wamejifukuzisha kazi.
Hata alipoingia wodini kuzungumza na wagonjwa, Naibu Waziri Jafo alielezwa kwamba huduma zinazotolewa hapo hususani nyakati za usiku ni duni.
 Kwa upande wake, Katibu wa Hospitali hiyo Leonard Lwesya Akitoa utetezi wake alisema kuwa,sababu ya kuendelea ni mfumo huo ni kutokana na mfadhili aliyeingiza mkataba na Wiraza ya Afya kufunga mfumo wa EFDs  bado hajakamilisha japo yupo hatua za mwisho.
 “Hii yote inatokana na ubadhirifu wa mapato hadi mnashindwa kununua mabomba ya sindano na groves, kwa sababu fedha zinaishia mikononi mwa watu wachache. Haingii akilini kabisa eti unaniambia kwa mwezi unakusanya Sh3 milioni hospitali kubwa kama hii?…. haiwezekani hapa kuna kitu ndio maana hamtaki kufunga mashine za kieletroniki,” alisema Jafo.
Nao wagonjwa waliolazwa katika Hospital hiyo walipata nnafasi ya kuzungumza waziri,ambapo, Julias Songella alisema  kuwa,wagonjwa wanaolazwa hospitalini hapo wanalazimika kila mmoja kwenda na mablanketi yake,kutokana na kukithiri kwa uhaba wa mashuka  katika Hospital hiyo.Pia alisema usiku hawapatiwi huduma nzuri kwani hata mabomba ya sindano yanakosekana.

 

Naibu waziri wa Tamisemi Suleiman Jaffo akiwa katika picha ya pamoja na walimu wahitimu

0 maoni:

Chapisha Maoni