Jumamosi, 10 Septemba 2016

WANAFUNZI SHULE YA MSINGI MLOWA ILULA WILAYA YA KILOLO WASOMEA CHINI YA MTI KWA KUKOSA VYUMBA VYA MADARASA TOKA KUANZISHWA KWA SHULE HIYO


Posted by Esta Malibiche on Sept10.2016 in News

Na Esta Malibiche 

Iringa

MKUU wa wilaya ya Kilolo mkoani Iringa Asia Abdalah amefanya ziara ya kushtukiza katika shule za Msingi zilizopo Halmashauri ya Mji mdogo wa Ilula  Mkoani Iringa ili kujiridhisha na mwenendo wa mitihani ya darasa la saba .
Katika ziara yake hiyo alitembelea shule ya Msingi Mazombe,Ilula,Isolikawaya,Masukanzi na Shule ya Msingi Ilindi na Mlowa  na kushuhudia hali ya utulivu na Amani uliotawala maeneo ya shule na vyumba vya madarasa ambayo wanafunzi hao huku wanafunzi wakimhakikishia kufanya vizuri mitihani yao.
Akizungumza na wanafunzi wa darasa la saba  katika sule ya Msingi Isoliwaya iliyopo kata ya Ilula Halmashauri ya Mji Mdogo wa Ilula,aliwasihi wanafunzi hao kuwa watulivu katika mitihani yao na mara wamalizapo darasa la saba wasitoloke kwenda mjini kufanya kazi za ndani bali  wajiandae kujiunga na kidato cha kwanza 2017 kama serikali inavyosema.
‘’’’Ninawasihi wanafunzi mtulie nyumbani  ili kujiandaa na kuingia kidato cha kwanza mwakani .Sitakubali kuona mnaenda kufunya kazi za ndani mjini na kupelekea kushindwa kuanza masomo ‘’’’
Akiwa shule ya Msingi Mlowa alibaini changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na  ukosefu wa vyumba vya madarasa katika shule hiyo hali iliyopelekea wanafunzi wa darasa la nne,la tatu na awali kusoma chini ya  miti toka kuanzishwa kwa shule hiyo mwaka 2009 mpaka hivi sasa2016
Dc Asia alichukizwa na hali hiyo iliyodumu  kwa muda mrefu bila kupatiwa ufumbuzi huku  wanafunzi wakiendelea kupata  adha kusomea katika mazingira magumu sana yasiyofaa ndani ya nchi yao. Baada ya kubaini hali hiyo aliahidi kutembelea kila shule ili kufanya ukaguzi wa mazingira wanayojifunzia wanafunzi .

‘’’Nimesikitishwa sana na ninapata kigugumizi kuona ndani ya miaka 8 toka shule hii kuanzishwa haijamaliziwa ujenzi wa vyumba vya madarasa.Hii changamoto nimeipokea kwa huzuni mkubwa na nimeichukua  kwa dharula na kuondoka nayo kwenda kukaa na wenzangu ili kujadili namna ya  kuchukua hatua za haraka ili kukamilisha ujenzi wa vyumba vilivyobaki  na hatimae wanafunzi waweze kusoma katika mazingira rafiki.Ninaenda kulifanyia kazi kwa haraka ili iweze kutatuliwa haraka iwezekanavyo ‘’’’’alisema Asia
Awali Mkuu wa shule hiyo Willium Willson akizungumza na mkuu wa Wilaya mara baada ya kuwasili katika shuleni hapo alisema kuwa licha ya kuwa na changamoto ya wanafunzi kusoma katika mazingira yasiyo rafiki chini ya mti,pia shukle hiyo inakabiliwa na uhaba wa walimu pamoja na vnyumba za walimu.
‘’’’’’’Shule hii inawanafunzi 100 na vumba vya madarasa ambavyo havijamalizika viko4 ambapo vyumba 2 bado havijakamilika toka  vianze kujengwa mwaka 2014.Tunasikitika kwamba tuna viongozi wa Wilaya akiwemo mbunge wetu,Lakini tunashangaa tunaona hii changamoto inayotukabili hap haata Mbunge wetu Mwamoto hajawahi fika hapa na kuangalia jinsi watoto wanavyoteseka kipindi cha masika kusomea chini ya miti kama unavyoona mkuu wa Wilaya’’’’’alisema Willson
‘’’’’’Kwa kweli mazingira haya siyo rafiki sababu kipindi cha baridi wanafunzi wa darasa la nne, la tatu na darasa la awali huwa wanapata shida kipindi cha baridi na mvua zinapoanza kunyesha’’’’alisema Wilson

‘’’’Walimu waliopo wako 7 ambao huwa tunajigawa namna ya kufundisha kuanzia awali hadi darasa la saba,hivyo tunaiomba serikali iweze kulianalia hili kwa haraka’’’’’’alisema Willson
MWISHO

0 maoni:

Chapisha Maoni