Jumamosi, 10 Septemba 2016

MKUU WA WILAYA YA BARIADI FESTO KISWAGA AMEWATAKA WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA KILELE CHA MBIO ZA MWENGE WA UHURU

Posted by Esta Malibiche on Sept10.2016 in News








Mkuu wa wilaya Bariadi mkoani Simiyu Festo Kiswaga amewataka wananchi wilayani humo kujitokeza kwa wingi katika kilele cha mbio za    mwenge wa uhuru kitaifa zinazotarajiwa kufanyika mwezi October 14.2016 wilayani humo.
Kiswaga alisema kuwa sherehe hizo zitakazoambatana na kumbukumbu ya baba wa Taifa na kilele cha wiki ya vijana Duniani.
Akizungumza na wananchi wa  bariadi katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana katika eneo la stendi ya zamani na kukagua na barabara eneo linalojengwa karavati ikiwa ni moja ya maandalizi.
‘’’Ninawaomba wananchi wa wilaya ya Bariadi tujiandae  kupokea ugeni mkubwa kutoka nje ya mkoa,ugeni wa kitaifa na kimataifa ili kuhakikisha sherehe zinafana na kufanyika kwa Amani na utulivu’’’’’alisema Kiswaga
Alisema Mwenge wa uhuru wilayani humo,unatarajia kuwasili October 12,ambapo utakimbizwa  bariadi mjini, October 13 utakimbizwa Halmashauri ya Bariadi na October 14 kilele cha mbio za mwenge kitaifa zitakazofanyika Bariadi Mjini ambapo mgeni rasmi anatarajia kuwa Rais wa awamu ya tano Dkt.John Pombe Magufuli.

Wananchi wa bariadi wakimsikiliza kwa makini mkuu wa wilaya hiyo katika mkutano uliofanyika jana





 Mkuu wa wilaya ya Bariadi akikagua karavati inayoendelea kujengwwa katika barabara ya baraiadi mjini ikiwa ni moja ya maandalizi ya kilele cha mbio za mwenge wilayani humo.

0 maoni:

Chapisha Maoni