Hospitali
ya Benjamini Mkapa ya UDOM mjini Dodoma imeanza kutoa huduma ya
matibabu ya ugonjwa wa Saratani kwa watoto wadogo kwa kushirikiana na
shirika lisilo la kiserikali la Marafiki wa Watoto wanaoishi na saratani
nchini – ‘friends of children with cancer’.
Mganga
mkuu wa mkoa wa Dodoma Dokta James Charles amewaambia waandishi wa
habari mjini Dodoma kuwa hosptali hiyo itatoa huduma ya kutibu ugonjwa
wa Saratani kwa wakazi wa Dodoma na mikoa ya kanda ya kati.
“Kama
mnavyofahamu katika mkoa wa Dodoma tunayo hospitali ya Benjamin Mkapa
na hospitali ya Mkoa wa Dodoma ambayo imeongezewa uwezo mkubwa na
tutaanza kutibu ugonjwa wa Saratani hususani katika kituo cha Benjamin
Mkapa” amesema Dk.James
Dk
James ameongeza kuwa huduma hiyo itatoa fursa kwa wakazi wa Dodoma na
mikoa ya kanda ya kati kupata huduma kwa wakati bila kukaa mda mrefu
wakusubiri matibabu.
Mkurugenzi
wa shirika la ‘Friends of Children with Cancer’ Janet Maloni na Makamu
wa Rais wa Shirika hilo wameelezea takwimu na uzoefu wao kuhusu hali
halisi ya ugonjwa saratani kwa watoto nchin.
“Tafiti
zinaonyesha kwamba Tanzania tunatarajia watu wanaopata saratani kwa
mwaka si chini ya watu 40,000 na kati ya hao 27,000 watapoteza maisha
bila kufika katika vituo vya afya” amesema Bi Janet
“Kwa
watoto tunatarajia watoto 2500 wanazaliwa na tatizo hili na wanaofika
katika vituo vya afya, kwa mfani kile cha Muhimbili sio zaidi ya watoto
500” ameongeza Janet
Kwa
mujibu wa Mganga Mkuu wa mkoa wa Dodoma Bw. James Charles amesema kuwa
ugonjwa wa saratani kwa watoto unatibika endapo mtoto atapatiwa huduma
na tiba sahihi mapema katika kituo husika cha matibabu ya saratani.
Na Hashim Ibrahim (UDSM-SJMC)
0 maoni:
Chapisha Maoni