…………………………………………
Ni
rahisi sana kutamka neno afya, neno hili linajenga dhana ya hali ya
ukamilifu kimwili, kiakili, kijamii na kutokuwepo kwa maradhi ambayo
huleta hali ya kuwa huru na kutokuwa na hali ya kuumwa au udhaifu wa
mwili.
Kuwa
na afya tu haitoshi, mwanadamu anapaswa kuwa na afya bora ambayo
huchukuliwa kama nguzo na raslimali muhimu katika kuchangia maendeleo ya
mtu binafsi, familia na nchi hususan katika kuleta maisha bora na
kupunguza umaskini.
Kwa
mantiki hiyo, afya bora inalenga kuwa na ustawi endelevu kwa jamii, kwa
kuzingatia mchango wa mtu binafsi kulingana na nafasi, uwezo na fursa
zilizopo katika kuleta maisha bora.
Upatikanaji
wa afya bora unahitaji uwezeshaji wa jamii yenyewe iwe na uwezo wa
kushiriki, kuamua, kupanga na kutekeleza mikakati yao ya kuwaletea
maendeleo katika ngazi mbalimbali.
Ili kuwa na afya bora ni vizuri kujiuliza maswali kadhaa ambayo ndiyo yatajenga msingi imara wa afya ya mtu binafsi au jamii.
Maswali
hayo ni pamoja na Unakula nini? Unakula kiasi gani? Unakula aina gani
ya vyakula? Una lala kwenye nini? Unalala masaa mangapi kwa siku?
Unafanya mazoezi? Unakula mara ngapi kwa siku?Unakunywa nini? Unapata
hewa safi unapokuwa kazini au nyumbani? Unapata muda wa kwenda hospitali
mara kwa mara kupima afya yako?
Maswali
haya ni ya msingi katika kujenga afya bora kwa kuzingatia elimu ya afya
na uhamasishaji miongoni mwa jamii unapaswa kuwa njia muhimu katika
utoaji wa huduma za afya.
Njia
hiyo inatumia utaalamu wa mawasiliano kwa kutayarisha na kuwasilisha
ujumbe mbalimbali kwa mtu binafsi, familia na jamii kwa lengo la
kubadilisha mienendo na tabia zinazochangia kuwepo au kutokuwepo kwa
maradhi katika jamii.
Hali
hiyo ya afya bora inapokuwa tofauti maana nayo hubadilika, watu wengine
husema “Ninaumwa, ninahoma, sijisikii vizuri, ni mgonjwa n.k”.
Misemo
hiyo ambayo hutumiwa kila mara huonesha mtu au jamii fulani afya yao
sio nzuri, mara nyingi watu hawa na wale anaojiona ni wazima wanasahau
wapo miongoni mwao wenye uzito mkubwa kupita kiasi ambapo hali hiyo
inawafanya waonekane wanene kupita kiasi ambao huo ni ugonjwa.
Unene
wa kupindukia hupelekea mwili kuwa na mafuta ya ziada ambayo
hulimbikizana hadi kiwango kinachoweza kuathiri afya na kupelekea
kupungua kwa matarajio ya mtu kuishi muda mrefu au kuwa na ongezeko
kubwa la matatizo ya kiafya.
Utafiti
mpya umeonesha watu wazima wengi duniani ni wanene kupita kiasi na
kwamba hakuna matumaini ya kufikia lengo la kupunguza idadi ya watu
wanene duniani.
Wanasayansi
waliofanya utafiti huo ambao walitoka Chuo cha Imperial cha London,
waliandika katika jarida la kimatibabu la Lancet la Uingereza, wanasema
miongo minne iliyopita, kuwa na uzani wa chini kupita kiasi lilikuwa
tatizo kubwa kuliko unene.






0 maoni:
Chapisha Maoni