Ijumaa, 8 Aprili 2016

MKAZI WA KIDAMALI IRINGA AHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA ...........


Mshitakiwa Bw Joseph Balami akipelekwa  mahabusu  ya muda katika mahakama kuu kanda ya  Iringa  leo  baada ya  kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa  kosa la  kumuua mwenzake  Stani Singaile  (42) katika  ugomvi  uliotokea  kwenye  kilabu cha pombe za  kienyeji kijiji  cha Kidamali Iringa (picha na MatukiodaimaBlog)
Mkazi  wa Kidamali  Iringa Bw Joseph Balami akiwa ametiwa hatiami kwa kuhukumiwa  kunyogwa hadi kufa baada ya  kupatikana na hatia ya mauwaji 
.................................................................................................................................................................................
MKAZI  wa Kidamali wilaya ya  Iringa mkoani Iringa Bw  Joseph Balami amehukumiwa  kunyongwa hadi kufa  baada ya  kupatikana na hatia ya  kumua  Stani Singaile (42) kwa  kumchoma kisu kusudi wakati wa ugomvi  uliotokea  kwenye klabu cha pombe za  kienyeji .
Hukumu hiyo  imetolewa  leo na mahakama kuu kanda ya Iringa imetoa  baada ya  kuridhishwa na ushahidi  uliotolewa mahakamani  hapo na upande  wa jamhuri  ambao ulidai  kuwa mtuhumiwa   huyo alitenda kosa hilo Oktoba 15 mwaka  2011 katika kijijhi cha Kidamali kwa  kumuua
 Stani Singaile  (42) .

 
Akisoma hukumu hiyo,Jaji Mfadhi wa mahakama Kuu kanda ya Iringa Bi Mary Shangali alisema katika shauri kesi hiyo amekubaliana na upande wa mashitaka ulidai ushhidi uliotolewa mahakamani udhihirisha pasipo shaka kuwa mtuhumuwa alitenda kosa hilo.
 
“Katika kesi hii upande wa mashitaka ulileta mashidi watano na upande wa utetezi ulileta mashahidi wawili ambao ni mtuhumiwa mwenywe na mke wake waliotoa ,ushahidi  mahakamani,mahakama imekubaliana na upande wa mashitaka kuwa mtuhumuwa ametenda kosa na imemtia hatiani kwa kosa la kuua kwa makusudi”alisema Shangali na kuongeza:
 
"Kwa  kuwa adhabu inayotolewa kwa kosahilo ni moja kwa mjibu wa sheria...,ninakuhukumu kunyongwa hadi kufa”alisema Shangali.
 
Awali kabla ya Hakimu kusoma hukumu hiyo mawakili  Felix Chakela upnde wa serikali na Lwezaula Kaijage upande wa utetezi walipewa nafasi ya kutoa hoja zao ambapo Chakela aliitaka mahakama kumpa adhabu kali mtuhumiwa ili iwe fundisho kwake na kwa watu wengine wenye nia ya kutenda kosa kama hilo wakati Lwezaula alisema anasubiri hukumu ya mahakama.
 
Awali Jaji huyo aliyekuwa akinukuu maelezoya awali ya kesi hiyo iliyofunguliwa mahgakamani hapo na wawili wa serikali …alidai  mtuhumiwa alitendokosa hilo Oktoba 15 mwaka 2011 katikakilab cha pombe za kienyeji.
 
Alisemakulingana na mashuhuda waliotoaushahidi mahakamani pa wamethibitsiha bilakuacha shakakuwa siku hiyo mtuhumiwa alikwenda kwenye kilabu kile na kumfuatamarehemu kisha kumchoma na kisu kifuani.
 
Alisema kitendo cha mtu kumfuata mtu na kumchoma kisu kifuani hususani upande wa kushoto kinaonyesha alidhamilia kua na kwamba kwatendohilomahakamainamtia hatini kwakosala mauaji ya kukusudia.
 
Pia aliongeza kuwa ushahidi uliotolewa  mahakamani hapo pamoja na maoni yaliyotolewa na waungwana wa mahakama yanakubaliana kuwa ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka haukuacha shaka kwa mtuhumiw akuhusika na tukio hilo.
 
Katika kesi hiyo mtuhumuwaBw  Balami anadaiwa kuwa Oktoba 15 mwaka 2011katika kijiji cha Kidamali Wilaya ya Iringa majira ya saa moja usiku alimua Singaile kwakumchoma na kisu ,tukio alilotenda kwenye kilabu cha pombe za kienyeji.
 
Alidawa mahakamani hapa na uapnde wa jamuhuri kuwa baada ya tukiomtuhumiwa alikimbia lakini alikamtwa majiraya saa mbili usiku na kufikishwa kwenye ofisi ya serikali ya kijiji na baadae katika kituocha polisi kwa hatua zaidi hata   hivyo  mahakama  hiyo  imesema kuwa  rufaa kwa ipo  wazi  kwa mshitakiwa   huyo.

0 maoni:

Chapisha Maoni