............
| Viongozi na wananchi wa kata tatu za Ilula wakiwa katika hafla ya makabidhiano ya mradi wa maji wa Idemule |
| Mwenyejkiti wa bodi ya IRUWASA Bw Mhongole kushoto akiwa na mbunge wa jimbo la Kilolo Bw Venanve Mwamoto |
| MkurugenzI wa IRUWASA Bw Gilbert Kayange akikabidhi taarifa ya mradi huo wa maji Ilula |
| Mkurungezi wa IRUWASA Bw Gilbert Kayange akitoa taarifa ya mradi huo |
| kaimu meneja wa mradi wa maji Ilula Bi Mvungi kushoto akiwa katika hafla hiyo |
| Zoezi la kusaini hati ya makabidhiano likiendelea |
| Baadhi ya maeneo ambayo mradi huo umekuwa ukihujumiwa |
MAMLAKA
ya maji safi na maji taka mjini Iringa (IRUWASA ) imekabidhi
maradi wa maji wa maji uliogharimu kiasi cha Tsh milioni 903kwa
mamalaka ya maji ya mji mdogo wa Ilula wilaya ya Kilolo mkoani
Iringa baada ya mradi huo ujenzi wake kukamilika huku mbunge wa
jimbo la Kilolo Venance Mwamoto akitaka wanasiasa kuacha kushikilia
andiko la mradi mkubwa wa maji katika mji wa Ilula
Akizungumza
katika hafla ya makabidhiano ya mradi huo wa maji jana mbunge wa
jimbo la Kilolo Bw Mwamoto pamoja na kupongeza wizara ya maji na
umwagiliaji kwa kusaidia kutoa pesa kwa ajili ya mradi huo bado
alieleza kusikitishwa kwa na hatua ya wanasiasa katika wilaya ya
Kilolo kushikilia andiko la mradi mkubwa wa maji katika mji huo na
kutaka nyaraka zote za miradi kuhifadhiwa na wataalam na sio
wanasiasa .
Kwani
alisema kuwa moja kati ya mambo ambayo yanachelewesha ufumbuzi wa
kudumu wa kero ya maji katika mji wa Ilula ni pamoja na baadhi ya
wanasiasa kuingiza siasa katika shughuli za kimaendeleo na kutaka
maandiko yote ya miradi ya maji katika wilaya ya Kilolo ambayo
yaliandikwa kabla ya yeye kuwa mbunge wa jimbo hilo kukabidhiwa na
kuhifadhiwa na watendaji wa mamlaka ya maji na si vinginevyo.
Mbunge
huyo alisema kuwa haungi mkono wazo la andiko la kutoa maji kwa
ajili ya mradi mkubwa kutoka chanzo cha maji cha Idemule kwani mradi
huo ni vigumu kutekelezeka na kuwa ni vema mradi mkubwa wa maji kwa
ajili ya wananchi wa mji wa Ilula ukatekelezwa kutoka mto Ruaha mjini
Iringa kuliko kutegemea chanzo hicho cha Idemule .
Alisema
kuwa tayari Rais Dr John Magufuli aliahidi kusaidia kutatua kero ya
maji katika mji wa Ilula wakati wa kampeni zake ila iwapo viongozi
wa maji na wale wa wilaya hiyo hawatakuwa wabunifu kwa kuangalia
uwezekano wa kutoa maji mto Ruaha mjini Iringa na kubaki na mawazo ya
wanasiasa ya kutaka maji hayo kutoka mto Idemule upo uwezekano wa
Rais kumaliza muda wake Ikulu pasipo mradi huo kutekelezeka .
"Naomba
kuwa wazi katika hili wapo baadhi ya wanasiasa wanataka
kukwamisha mradi huo mkubwa wa maji katika mji wa Ilula haiwezekani
kwa mamlaka ya maji Ilula kumwachia mwanasiasa kutunza andiko la maji
wakati si jukumu lake ...siasa inayoendelea Ilula na wilaya ya kilolo
haina faida yeyote kwa wananchi ......hivyo ili mradi huu mkubwa
uweze kutekelezeka kwa wakati ni vema wataalam kuachwa kufanya kazi
za kitaalam na wanasiasa kufanya siasa "
Alisema
kuwa sida kubwa hata ya miuondombinu ya maji katika mradi huo
kuendelea kuhujumiwa ni siasa chafu zinazofanywa na baadhi ya
wanasiasa kwa ajili ya kinyongo cha kukosa nafasi walizotegemea katika
siasa .
Akitoa
taarifa ya mradi huo mkurugenzi wa IRUWASA Bw Gilbert Kayange
alisema kuwa mradi huo utahudumia kata tatu za mji wa Ilula ambazo
ni Nyalumbu , Ilula na Lugalo ambapo wakazi 38,265 ambao alikuwa
wakikabiliwa na kero ya maji kabla ya wizara ya maji na umwagiliaji
kutoa kiasi cha Tsh milioni 860 kwa ajili ya kutatua kero hiyo na
kuwa hadi sasa mradi huo unadaiwa kiasi cha tsh milioni 43ambazo ni
pesa kwa ajili ya kumlipa mkandarasi wa ujenzi wa mradi kutokana na
kazi alizofanya .






0 maoni:
Chapisha Maoni