Jumamosi, 2 Aprili 2016

LUHWAVI: WATUMISHI WA CHAMA CHACHU YA CCM KUNG’ARA KATIKA JAMII

Na Bashir Nkoromo, Njombe
………………………………………………
Watumishi wa Chama ni sehemu muhimu inayokifanya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuendelea kuwa bora na imara kwa kuwa ndiyo jiko la kubuni na kuandaa taswira ya muonekano wa Chama katika jamii.
Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Rajabu Luhwavi wakati akizungumza na watumishi wa Chama Cha Mapinduzi kutoka wilaya za mkoa wa Njombe na Ruvuma, jana, akiwa katika ziara ya kikazi katika mkoa huo kuzungumza na kusikiliza changamoto na kero zinazowakabili watumishi wa Chama. 
Alisema, ni kutokana na kutambua umuhimu wa watumishi hao ndiyo sababu Chama Cha Mapinduzi kinafanya kila jitihada kuhakikisha kinakutana nao ili kujua mazigira walioyomo na changamoto na kero zinazowakabili ili kuweza kutafuta njia za kuzitatua kwa kadri inavyowezekana.
“Unajua mimi ndiyo nasimamia utumishi katika chama, kazi zingine zote zinazonihusu naweza kuzifanya kupitia mafaili nikiwa ofisini, lakini hili la kuhusu mazingira na hali za watumishi ambalo pia linanihusu siweze kulifanya nikiwa ofisini, ndiyo sababu nimeamua kufanya ziara hizi, ili niwasilikilize kero na changamoto zinazowakabili tukiwa pamoja”, alisema Luhwavi.

0 maoni:

Chapisha Maoni