Jumamosi, 3 Septemba 2016

Samsung yatangaza kusimamisha moja ya bidhaa zake


Kampuni maarufu duniani ya Samsung inayotengeneza vifaa mbalimbali vya kielektroniki kama Jokofu, Televisheni, Redio, na Tanakilishi pamoja na vitu vingine imesema kuwa itasitisha uuzaji wa moja ya vifaa vyake ambacho ni simu ya mkononi aina ya Galaxy note 7
Hatua hiyo imechukuliwa baada ya  ripoti kutoka  Marekani na Korea Kusini kueleza kwamba simu hizo zimekuwa zikilipuka wakati au baada ya kuwekwa chaji kwenye umeme.
Tukio hili limejiri ikiwa ni wiki moja tu kabla ya mshindani wake mkuu katika soko la biashara ya kielektoniki Apple kuzindua toleo lake jipya la simu aina ya iPhone.
Mapema siku ya Jumatano ya tarehe 31 Agosti, kampuni ya Samsung ilisema imesitisha usafirishaji wa simu hizo kwa kampuni tatu kuu zinazosafirisha simu hizo maeneo mbalimbali duniani ili kufanya uchunguzi zaidi. 
Na Hashim Ibrahim (UDSM-SJMC).
SAMSUNG N7
Moja ya bidhaa hizo zikiwa tayari zimelipuka baada ya kuchajiwa..
SAMSUN NN7

0 maoni:

Chapisha Maoni