WANAFUNZI 65 wa shule ya
sekondari chalinze iliyopo Wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wamenusurika
kupoteza maisha baada ya bweni moja la kulalia kuteketea kabisa kwa
moto wakati wao wakiwa darasani kwa ajili ya kujisomea masomo ya usiku.
Akizungumza na mwandishi wa
habari hizi Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga kuhusina na tukio
hilo alisema kwamba limetokea jana majira ya saa 3:20 usiku wakati
wanafunzi hao wakiwa madarasani wanajisomea.
Mkuu huyo alibainisha kwamba
chanzo cha moto huo inadaiwa ni shoti ya umeme ambayo imesababisha moto
huo kuteketeza vifaa vyote vikiwemo magodoro,vitanda,vitabu
vilivyokuwemo katika bweni hilo ambalo lilikuwa likilaliwa na wanafunzi
wapatao 65 wa kiume.
“Taarifa za awali ambazo
tumezipata chanzo cha kuungua kwa jengo hili ni umeme, lakini kwa kweli
ni tukio la kusikitisha kwani vifaa vyote na mali za wanafunzi hao 65
ikiwemo magodoro,vitanda, madatfari yao yote yameteketea kwa moto
huo,”alisema Mwanga.
Aidha Mwanga akizungumzia
kuhusina na juhudi za serikali ambazo tayari wameshazichukua hadi sasa
ikiwemo kuwahifadhi wanafunzi hao 65 katika jengo lingine kwa muda
wakati wanaendelea na jitihada zingine za kuangalia ni namna gani ya
kulijenga jengo linguine kwa haraka.
Alisema kuwa kwa sasa kutokana
na tukio hilo la kuungua kwa shule hiyo amewaomba wadau mbali mbali wa
maendeleo kujitoa kwa hali na mali kutoa michango yao kwa ajili ya
kuwezesha ujenzi mwingine wa jengo hilo ikiwemo na mahitaji ya msingi
wanayostaili kusaidiwa wanafunzi hao waliounguliwa na mali zao.
Katika hatua nyingine alisema
kwamba baada ya moto huo kutokea hakukuwa na msaada wowote wa gari ya
zima moto hivyo kuliweza kuchangia kwa kiasi kikubwa kuendelea kushika
kasi ya moto na kuteketeza vitu vyote katika jengo hilo, ambapo jitihada
za kuuzima zilifanywa na jeshi la posili viongozi wa serikali pamoja na
wananchi wenyewe.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa
mamlaka ya mji mdogo Chalinze Hussein Mramba amekiri kutokea kwa tukio
hilo ambapo alisema kwamba mkakati waliyojiwekea ni kushirikiana na
wadau wa maendeleo ili kuweza kuhakikisha kwamba wanajenga jengo
linguine ili wanafunzi waweze kupata sehemu ya kulala.
SHULE hiyo ya sekondari
Chalinze iliyopo wiayani bagamoyo Mkoa wa Pwani ina jumla ya idadi ya
wanafunzi 1151.ambapo kati yao 65 kwa sasa wameunguliwa na vitu vyao
vyote hivyo kunahitajika juhudi za serikali katika kuhakikisha wanatoa
msaada wa hali na mali ili waweze kuendelea masomo yao.
0 maoni:
Chapisha Maoni