Alhamisi, 7 Aprili 2016

UJUMBE WA TUME YA UCHAGUZI YA ZIMBABWE WAJA KUJIFUNZA NEC

KAI2
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damiana Lubuva akisalimiana na Catographia Bwana Brian Mhonda toka Tume ya Uchaguzi Zimbabwe walipofika ofisi kwake kusalimiana naye. Katikati toka kushoto ni Kaimu Mkuu wa sehemu ya Catographia toka Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bwana Adolph Kinyero na Afisa Uchaguzi wa Wilaya Toka Tume ya Uchaguzi Zimbabwe Collins Chamunorwa Muchenjekwa
KAI1Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bwana Kailima Ramadhani,akizungumza na Kaimu Mkuu wa Catographia kutoka Idara ya Daftari Bwana Adolph Kinyero muda mfupi baada ya kupokea ujumbe wa Maafisa Uchaguzi toka Tume ya uchaguzi Zimbabwe Ofisini kwake. Waliokaa katikati toka Kushoto ni Catographia wa Tume ya uchaguzi Zimbabwe, Bwana Brian Mhonda na Afisa Uchaguzi wa Wilaya Bwana Collins Chamunorwa Muchenjekwa.
………………………………………………………………………………………………………………………..
Na Christina Njovu-NEC
Ujumbe kutoka Tume ya Uchaguzi ya Zimbabwe (ZEC) umekuja kujifunza kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) jinsi ilivyoendesha zoezi la Uandikishaji Wapiga Kura kwa kutumia Mfumo wa Biometrick Voter Registration (BVR) kwa kuwa Tanzania   ilifanikiwa kwa kiasi kikubwa kuandikisha wapiga Kura wengi kwa kutumia technologia hiyo mpya.
 Wakizungumza na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mh. Jaji Mstaafu Damian Lubuva ujumbe huo wa watu wawili Brian Mhonda na Collins C. Muchenjekwa toka Tume ya Uchaguzi ya Zimbabwe wameeleza kuwa; Zimbabwe ipo katika maandalizi ya kuandikisha Wapiga Kura.
Ujumbe huo umeeleza kuwa; Zimbabwe imeichagua Tanzania nchi ambayo imefanya uandikishaji wa Wapiga Kura hivi karibuni na kufanikiwa kuandikisha watu wengi kwa muda mfupi kwa kutumia mfumo wa BVR.
“Tupo katika maandalizi ya kuandikisha Wapiga Kura kwa kutumia mfumo wa Biometric Voters Registration (BVR) mfumo ambao Tume yetu imeuchagua kutokana na kukua kwa Technolojia duniani” Mfumo huu kwa Zimbabwe utatumika kwa  mara ya kwanza” alisema bwana Muchenjekwa.
Wakiwa katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ujumbe huo ulijifunza namna  Elimu ya Mpiga Kura ilivyotolewa kiasi cha kuwafikia watu wengi ambao walijitokeza kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. 
Katika Ziara hiyo ya mafunzo,wajumbe hao  walihitaji kujifunza zaidi njia na mbinu mbalimbali za kutoa Elimu ya Mpiga Kura ili iweze kuwafikia wananchi wengi ili   wajitokeze kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
Sambamba na hilo walijifunza namna ya kusoma ramani ya Majimbo ya Uchaguzi na Jinsi gani Tume ilifanya manunuzi ya vifaa vya Uandikishaji wa Wapiga Kura.  
Ujumbe huo ulijikita zaidi katika kujifunza jinsi Biometrick Voter Registration (BVR) namna inavyofanya kazi pamoja na changamoto zake. 
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva amewapongeza kwa kuchagua kuja kujifunza nchini Tanzania kwani kitendo hicho  kinaipa heshima NEC na Tanzania kwa ujumla.

0 maoni:

Chapisha Maoni