Ijumaa, 8 Aprili 2016

Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela amewataka wananchi kutunza mazingira ili kuendana na mabadiliko ya tabia ya nchi



Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela  amewataka wananchi kutunza  mazingira ili kuendana na  mabadiliko  ya tabia ya nchi
Akifungua semina ya mabadiliko ya Tabia ya Nchi iliyoandaliwa na Muadhiri wa chuo kikuu cha kilimo sokoine [sua]kilichopo mkoani Morogoro  kwa kufadhiliwa na shirika la  UNCERTAINTY REDUCTIONIN MODELS FOR UNDERSTANDING DEVELOPMENT APLICATION[UMFULA] iliyowahusisha wadau mbalimbali kutoka mkoa wa Iringa na Njombe, iliyofanyika Mkoani Iringa  ,alisema kuwa kutokana na  mabadiliko ya tabia ya nchi,Nchi imejikuta ikikumbwa na changamoto mbalimbali kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na kuleta athari kubwa katika jamii na Taifa kwa ujumla

Kasesela alisema mabadilikohato yameleta athari kubwa nchini ikiwa nipamoja na mafuriko na kubolewa nyumba baadhi ya wananchi,ambapo hali hii imesababishwa na kutojiandaa mapema  kiutafiti.

“””Nchi yetu inatatizo kubwa la kukumbwa na majanga mbalimbali,hivyo kama tutaweza kufanya utafiti  mapema na kuwa na maandalizi ya kutoshereza kujikinga au kuzuwia  majanga halii hii haitatokea tena

Tunapofanya utafiti tunatakiwa tutengenze uataratibu wa kushirikiana na jamii tuanzishe mapambano ya kupokoa mazingira yetu.

Jafet Kashagila ni muadhiri katika chuo kikuu cha kilimo sokoine [SUA] kilichopo mkoa Morogoro ambae ndiye muandaaji wa semina hiyo alisema kuwa lengo la kuandaa semina  kuhusu utafiti wa mabadiliko ya tabia ya  nchi ni kwaajili ya kuzalisha takwimu mbalimbali zitakazowezeza isaidia serikali ili iweze kukabiliana na changamoto inayoikabili  kuhusu athari zinazotokana na mabadiliko ya Tabia ya nchi.

Kashagila alisema asilimia kubwa ya shughuli zinazowafanywa na binadamu zimechangia kwa kiasi kikubwa kuleta mabadiliko ya Tabia ya nchi kutokana na kuharibika kwa vyanzo vya maji.

‘’’’Sisi tunataka kufanya utafiti utakaoelezea hali Fulani ya hali ya hewa ,joto pamoja na  mvua ili kutambua uhalisia wa eneo husika’’’’’alisema

Kwa hiyo mradi huu wa UNCERTAINTY REDUCTIONIN MODELS FOR UNDERSTANDING DEVELOPMENT APLICATION[UMFULA]ambao umetufadhiri kufanya utafiti wa mabadiliko ya tabia ya nchi,tutajitahidi wadau  kwa kupitia muunganiko  huu wa ushirikishwaji utatusaidia kupata taarifa mapema na kwa wakati kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa na hatimae serikali kuyafanyia kazi haraka iwezekanavyo’’’alisema

Katika maipango yetu tumejipanga baada ya utafiti tutatoa taarifa iwasaidie serikali na kuleta uwelewa mzuri wa mabadiliko’’’alisema

Tutashirikishana kuanzia mwamzo  na katika kila hatua ambayo tuatafikia taarifa kwa jamii pamoja na wadau  itatolewa   na hatimae kupata matokeo sahihi’’’alisema


0 maoni:

Chapisha Maoni