Jumanne, 12 Aprili 2016

HAJI MNASI AFISA ELIMU MSINGI MANISPAA IRINGA AINGIA DARASANI KUFUNDISHA



AFISA Elimu Msingi Manispaa  ya Iringaa Haji Mnasi ameungana na  walimu wake kuingia darasani na kufundisha ikiwa  ni utekelezaji wa mataala kwa vitendo.
Akizungumza na mtandao huu wa kali ya habari leo hii katika ofisi kwake alisema kuwa  ameamua kufundisha ili kuwatia moyo walimu wake katika zoezi la ufundishwaji.
Mnasi alisema  akiwa Afisa Elimu pia kitaaluma ni mwalimu,hivyo katika uataratibu alioupanga kwa kushirikiana na walimu katika viakao vya kazi atahakikisha anaingia darasani katika shule tofauti zilizopo ndani ya manispaa yake ili kuwaongezea maalifa wanafunzi ambayo  wanapewa na walimu wao
Miongoni mwa shule alizoingia na kufundisha nipamoja na shule ya Msingi Shule ambazo ameingia na Sabasaba,Njiapanda,Mlangali,Maendeleo ,Azimio pamoja na shule ya Msingi Kihesa hizi zote zipo ndani ya manispaa yake.
‘’’’’Mimi ni mwalimu kitaaluma,hivyo sina budi kushirikina na walimu wangu kuifundisha  ili kuendana na kasi yam h. rais wetu dkt John Pombe Magufuli kwa kutokukaa ofisini siku zote na kuzungusha kiti bila kuzunguka katika maeneo ya shule zangu na kuangalia changamoto zinazowakabili walimu na wanafunzi ‘’aliasema mmas
Aidha Afisa Elimu alisema  katika Halmashauri ya Manispaa  ya Iringa  inajumala ya shule za msingi 50 zikiwemo   shule za serikali 43,zenye wanafunzi 25133 wakiwemo  wavulan 12352 na wasishana 12781 na  kwa shule zisizo za serikali ziko 7,idadi ya wanafunzi wako 3347,wakiwemo wavulanan 1622 na wasichana 1725.
 Alisema jumla ya walimu katika shule za serikali wako 778 wakiwemo wanaume 150,na wanawake628 ,na kwa  shule zisizo za serikali zina walimu 129 wakiwemo wanaume 62,na wanawake67.
Alisema tangu Mh. Rais atangaze Elimu bila malipo Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imepokea kiasi cha Tsh.69,049,00/ kwa awamu ya tatu  yaani Desembailipokea  jumla ya 23,954,000,Januari ilipokea jumla 23,115,000 na Februari ilipokea jumla ya kiasi cha Tsh.21,980,000,hizi zote zimetumika kama ilivyopangwa.
‘’’’Pamoja na mafanikio hayo,katika shuguli za  utekelezaji wa utoaji Elimu  tumekuwa tukikabiliwa na chanamoto  mbalimbali ikiwemo uchakavu wa miundombinu ya baadhi ya shule ambazo zina umri mkubwa,msongamano wa wa watoto hasa kwa madarasa ya awali na la kwanza kama matokeo ya Elimu bure na kupelekea upungufu wa madarasa,madawati na vyoo, pamoja na ufinyu wa bajeti kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu hususani ya majiko na mahali pa chakula kwa wanafunzi’’’alisema
‘’’’’’Tumepanga mikakati kuakabiliana na changamoto hizo ambayo ni kuhakikisha tunatengeneza madawati mapya 2,803 kwa sasa madawati 1150 ytayari yanatengenezwa,kukarabati madwati yaliyochakaa,kuitisha harambee itakayoshirikisha wadau mbalimbali ili kuchangia madawati na ujenzi wa  wa nvyumba vya madarasa pamoja na kutafuta wafadhiri ndani na nje ya manispaa ya Iringa’’’’alisema




0 maoni:

Chapisha Maoni