Mbunge wa Kilombero Peter Lijuakali afanya mkutano na wafanyakazi wastaafu wa Illovo wa Kilimo cha miwa mapema jana Aprili 17.2016.
Katika mkutano huo, Mbunge huyo Peter Lijuakali aliweza kukutana na Wazee wa Kidatu na kujadiliana nao namna ya kumaliza mgogoro wa Wafanyakazi wastaafu wa kiwanda cha Miwa  cha Illovo pamoja na suala zima la kilimo cha miwa.
Pia aliweza kujadiliana nao mambo ya Afya, kilimo kwa ujumla na mambo mengine mengi ya kimaendeleo katika jimbo hilo.
“Changamoto za jimbo ni nyingi sana kiasi kwamba ninashawishika kuamini kuwa Kilombero ni kama haikua na Mbunge kabisa. Hatua kwa hatua tutazikabili changamoto hizi” alieleza Peter Lijuakali katika taarifa yake wakati alipokutana na wananchi wa jimbo lake hilo.
Peter Lijuakali amekuwa mstari wa mbele katika kufanikisha kuleta maendeleo ndani ya jimbo lake hilo tokea achaguliwe kwani amekuwa akisaidiana na wananchi katika shida na mambo mbalimbali  ya kijamii.
12524169_1076497482411962_541192808675383439_nMbunge wa Kilombero, Mh. Peter Lijuakali akiwa katika mikutano ya Wananchi wa jimbo lake hilo la Kilombero.12994558_1080122658716111_215033908333004837_nBaadhi ya wananchi na Wazee wastaafu wa kilimo cha miwa wakimsikiliza Mbunge wa jimbo hilo Mh. Peter Lijuakali.
944937_876989979078403_1171233164263762501_nMbunge wa kilombero akisalimiana na baadhi ya wafanyakaiz wa ujenzi wa Daraja lililokatika na kutenganisha barabara iliyopo jimbo la Kilombero Mang’ula B. 
13007248_877436219033779_8776899272979083869_nMbunge wa jimbo la Kilombero akipata nasaha za Wazee wa jimbo hilo la Kilombero…