MBUNGE wa
Jimbo la Kalenga Mkoani Iringa kupitia chama cha mapinduzi ccm Mh, Godfrey Mgimwa Alisema katika kukabiliana na tatizo la
vifo vya Wajawazito na Watoto wachanga tayari ameanza kupeleka dawa kwa baadhi
ya vituo vya afya katika jimbo lake ikiwa ni pamoja na kuboresha vituo
vya afya ambapo vituo takribani vinne vimekwisha kamilika.
Mgimwa aliyasema hayo katika
mahojiano maalum na mtandao huu wa kali ya habari alipotakiwa kueleza utekelezaji wa
majukumu yake tangu alipo chaguliwa kuwa Mbunge wa jimbo hilo.
Alisema kuwa uboreshaji wa huduma za
afya unakwenda sambamba na kuwapo wataalamu wa kutosha ambapo kwa nafasi yake
amekwisha kuanza hatua ya kuiomba serikali kuongeza wataalam katika jimbo lake
na kuvitaja vituo vya afya ambavyo vimekarabatiwa kuwa ni kituo cha afya Nzihi,
Mgama, Kiponzelo na Hospitali ya Tosamaganga ambayo inahitaji gari la kubebea
wagonjwa kutokana na gari lililopo kuwa dogo na kwamba halitoshi.
Alisema amejipanga katika bunge la
bajeti lijalo kulisemea swala la miradi na kuhakikisha bajeti inayopangwa
inakidhi mahitaji ya jamii ambayo pamoja na mambo mengine itasaidia pia
kuimarisha huduma za afya ya wajawazito na watoto wachanga
“Nimejipanga
vizuri kulisemea tatizo hili pamoja na miradi iliyopo kwenye jimbo langu kama
vile mradi wa maji Welu na Kiwele ambao haujakamilika ili ipangwe bajeti
itakayokamilisha mradi huo kwa ajili ya jamii. Tuna barabara na pia ambazo
nitahakikisha fedha zinatoka kwa ajili ya ujenzi huo na pia tutaboresha
mawasiliano ya simu ili kuwarahisishia wananchi kupata taarifa kwa wakati
pamoja na kuendelea kukamilisha mradi wa umeme vijijini” alisema Mgimwa
‘’Kuhusu Tanzania kuwa na Idadi
kubwa ya vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi Mgimwa amesema atahakikisha
anaweka mpango mkakati kwa kusimamia vipaumbele vyake kwa kushauri
serikali kutenga Fedha za kutosha ili kuweza kuboresha huduma za afya kwa akina
mama na watoto wanapozaliwa wawe na afya nzuri na pia kuwawezesha wazee nao
kupata huduma bora kwani wao wanastahili pia” alisema
Alisema mama mjamzito hatakiwi kusumbuliwa
kwa namna yeyote ambapo anatakiwa kupata huduma bora kwa ajili ya kulinda afya
yake
“Mwanamke mjamzito hatakiwi
kusumbuliwa kabisa na kwa namna yeyote na kwa
kulitambua hili mimi kwenye jimbo langu ninaweka mfumo utakaowasaidia
akina mama kwa haraka na kwa ubora zaidi ili wasipate shida’’.
Mgimwa alisema ongezeko la watu
haliwezi kuathiri mipango ya serikali bali linatakiwa kuwekewa mipango endelevu
ya bajeti itakayokidhi ongezeko la watu na kwamba tatizo siyo ongezeko bali ni
namna ya kukabiliana na ongezeko hilo kwa kuweka mipango ya huduma.
“Jambo la msingi ni kuweka
mkazo juu ya swala hili la ongezeko la watu ili wanapoongezeka waweze
kuongeza maendeleo ya taifa. Inatakiwa tuweke mazingira mazuri ili
wanapoongezeka wapate huduma muhimu, kwa mfano tunaweza kuwekeza katika elimu
ili wanapoongezeka wapate elimu kwa ajili ya maendeleo ya taifa” alisema.
Hata hivyo alisema uzazi wa mpango
si suala la kulisemea sana kimpango kwa sababu lina mambo mengi kutokana na
magonjwa na vifo.
“Hatuwezi kusema tunapunguza ili
twende na bajeti ila tunatakiwa kujipanga. Tujifunze kwa taifa la Nigeria lina
idadi ya watu wengi lakini uchumi wao upo vizuri pia tuangalie Marekani ina
watu wengi lakini uchumi wao ni mzuri. Cha msingi ni kuweka mipango ya kuimarisha
uchumi ili uendane na ongezeko la watu” alisema mgimwa.
|
0 maoni:
Chapisha Maoni