Jumatano, 20 Aprili 2016

KAMPENI YA CHANJO YA MINYOO KWA WATOTO CHINI YA MIAKA MITANO

images (2)
Na Masanja Mabula –Pemba 
WAKATI  kampeni ya utoaji wa Matone ya Vitamin ;A; na Dawa za Minyoo kwa watoto waliochini ya miaka mitano ,   likitarajia kufanyika tarehe 23 mwezi huu , uteuzi wa watendaji kwa ajili ya zoezi hilo umelalamikiwa na  baadhi ya masheha wa Wilaya ya Wete wakidai umefanyika kwa kujuwana .
Wakizungumza na Maofisa wa Wizara ya Afya Wilaya hiyo katika ukumbi wa mikutano wa Mkuu wa Wilaya hiyo , walisema baadhi watendaji (Cops)  wateuliwa  bila ya masheha kushirikishwa jambo ambalo huenda likaleta usumbufu wakati wa zoezi lenyewe.
Awali Afsa wa Afya Wilaya hiyo Ali Rashid Said alisema kuwa maandalizi yote kwa ajili ya kampeni hiyo yamekamilika ikiwa ni pamoja na vifaa kusambazwa vituoni na watendaji wakiwa wameandaliwa wamepatiwa mafunzo .
Alisema kila kituo kutakuwa na wafanyakazi wanne , wawili ni madaktari . mmoja cops pamoja na sheha wa Shehia husika ambao watashirikiana katika kazi kwa muda wa siku nne .
Sheha wa Shehia ya Fundo Jimbo la Gando Khamis Abeid alisema COPS walioteuliwa wanaweza kusababisha kutofanikiwa kwa zoezi hilo , kwani sio ambao walizoeleka kufanya kazi hizo .
“Cops aliyeteuliwa kufanya kazi katika Sheha yangu , sio yule wa zamani , na hii inaweza kusababisha kutofanikiwa kwa zoezi hili , huyo aliyeteuliwa amechaguliwa kwa mtindo wa kujuwana kwani mimi kama sheha sina taarifa juu ya uteuzi huu ”alieleza.
Naye Sheha wa Shehia ya Bopwe , Ramia Said Rashid aliishauri Wizara ya Afya kuacha kuchagua watendaji amba wanauhusiano nao , bali wawashirikishe masheha kuwapata kwani wapo waliozoeleka kifanyika kazi hiyo .
Alisema kwamba uteuzi huo uliofanywa na Wizara ya Afya utazua hisia tofauti kwa wananchi katika Shehia hiyo na kufahamisha kwamba hatakuwa tayari kubeba lawama ambazo hasitahili kuzibeba .
Aidha Sheha wa Mtemani Ali Juma aliutupia lawama Uongozi wa Wizara ya Afya Wilaya hiyo kwa kushindwa kuwashirikisha katika uteuzi Ili kupata  maoni ya masheha kwani Cops walioachwa wamekuwa wakijitolea kwa kipindi kirefu .
“Kwenye maslahi hatukushirikishwa ,  naomba uteuzi huu ukifanyika mara ya pili ni lazima wawangaliwe na kupewa kipaumbela cops ambao wamefanya kazi siku kwa njia ya kujitolea ”alishauri .
Katika mazungumzo yake na masheha afisa wa lishe wilaya hiyo Sabahi Khalfan alisema kwamba tayari Wizara imeandaa fomu maalumu ambazo Cops wanatakiwa kujaza wakati wa zoezi la awamu ijayo .
“Ili kuondoa malalamiko ya aina hii , wizara imeandaa fomu ambao kila cops atajaza , na hii itapunguza malalamiko , lakini kwa mara hii tunaomba tushirikiane pamoja na ili tufanikishe kwani hili ni suala la Kitaifa ” alisisitiza.
Aliwaomba masheha kutoa ushirikiano kwani wanahitaji kupata mafanikio katika zoezi hilo la kitaifa kwa kuhakikisha wanashiriki kazi ya uhamasishaji ili watoto waliolengwa waweze kufikishwa vituoni kupata matone na dawa za minyoo .

0 maoni:

Chapisha Maoni