Jumatano, 11 Januari 2017

HALMASHAURI YA MUFINDI YAPANDISHA UFAULU WA SHULE ZA MSINGI

Posted by Esta Malibiche on JAN 11,2017 in NEWS

Na Ofisa habari Mufindi
Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imeendelea kustawi katika sekta ya elimu  ambapo tathimini ya  matokeo  ya darasa la saba ya Halmshauri hiyo   yanaonesha kupanda kutoka asilimia 80.39 mwaka 2015  hadi  asilimia 84.90% mapema mwaka jana, ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 4.51.

Akisoma taarifa wakati wa kikao cha tathimini ambacho huwakutanisha wakuu wa shule zote za msingi na maaofisa elimu kata, Ofisa elimu taaluma wa Halmshauri ya Wilaya ya Mufindi MRIAMU NGALA amebainisha, kuwa tathimini ya ufaulu huo umejumuisha shule 143, watahiniwa elfu 05 mianne 38 ambapo wavulana ni elfu 02 miatatu 84 na wasichana ni elfu 03 na 54 huku wanafunzi waliofaulu na kuchaguliwa kuendelea na elimu ya Sekondari  wakiwa ni elfu 460 sawa na asilimia 84.9.

Bi. NGALA ameainisha masomo ambayo wanafunzi wamefanya vizuri zaidi kuwa ni pamoja na somo la Kiswahili ambalo  ufaulu wake  ni  asilimia 90. 51, Sayansi 90.13, Maarifa 87.88, Hisabati 56.34 huku somo la Kingereza likishika nafasi ya tano kwa asilimia 27.20

Aidha, afisa elimu huyo mwenye dhamana ya taaluma, ametaja baadhi ya malengo ambayo walijiwekea na ndiyo yaliyochangia kufikia mafanikio hayo kuwa ni pamoja na kufaulisha kwa asilimia 95, ufuatiliaji wa utendaji kazi, uwepo wa kambi za masomo, udhibiti wa utoro wa Wanafunzi na Waalimu, ukamilishaji wa mada kwa wakati na uwepo wa mazoezi ya kujipima.
Idara ya elimu msingi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imeweka uratibu wa kufanya tathimini ya kina kwa kila mwaka mara baada ya kutoka kwa matokeo ya mitihani ya darasa la saba ili kuangazia mafanikio ya ufaulu kwa kila shule, kubainisha changamoto na kuziwekea mikakati ya kuzikabili huku tathimini hiyo ikienda sanjari na kutunuku zawadi na vyeti kwa wakuu wa shule na maofisa ilimu kata walifaulisha wanafunzi wengi zaidi hivyo kupandisha wastani wa ufaulu wa halmashauri.




0 maoni:

Chapisha Maoni