Jumatano, 25 Januari 2017

VIONGOZI WA SERIKALI YA VIJIJI WAAGIZWA KUSOMA MAPATO NA MATUMIZI IRINGA

Posted by Esta Malibiche on JAN 26,2017 IN NEWS

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela akizungumza na wenyeviti wa vijiji, watendaji wa vijiji, watendaji wa kata, tarafa pamoja na wakuu wa idara wa halmashauri ya Wilaya ya Iringa kuhusu utekelezaji wa kodi ya majengo kwa vijiji wakati wa kikao cha kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Iringa jana.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Mahuninga, Kata ya Mahuninga wilayani Iringa, mkoani Iringa Lonjino Mkwele akimuuliza swali Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela (hayupo pichani) kuhusu utekelezaji wa kodi ya majengo kwa vijiji wakati wa kikao cha kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Iringa jana.


Mkutano ukiendelelea katika ukumvbi wa siasa ni kilimo,uliowahusisha viongozi wa serikali ya vijiji,watendaji wa vijiji,wantendaji wa kata kata,tarafa pamoja na wakuu wa Idara wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa.

VIONGOZI wa vijiji vyote wa Wilaya ya Iringa, mkoani Iringa waagizwa kusoma mapato na matumizi ili kuwarahisishia wananchi kufahamu jinsi fedha zao zinavyotumika na kutoa fursa kwa wananchi kupata nafasi ya kuhoji ili kujiridhisha pale wanapokuwa na mashaka.
 
Agizo hilo limetolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Iringa (DC), Richard Kasesela wakati wa mkutano na wenyeviti wa vijiji, watendaji wa vijiji, watendaji wa kata, tarafa pamoja na wakuu wa idara wa halmashauri ya Wilaya ya Iringa .
 
Kikao hicho cha kazi kililenga kuwakumbusha wenyeviti na watendaji wa vijiji na Kata kutambua majukumu yao na kuyapatia majibu sawia pamoja na swala zima la ukusanyaji mapato .

DC Kasesela ameagiza kufanyanyika uchunguzi ili kubaini kama kuna watendaji waliohamishwa kazi na wanatuhumiwa kuhujumu mapato ya serikali na michango ya wananchi kwa ajili ya shughuli za maendeleo kurudishwa haraka. 

Mkuu huyo wa Wilaya amewaagiza watumishi wote wa serikali ngazi ya Vitongoji, Vijiji na Kata kufanya kazi kwa haki, Usawa na uwazi na kiwashirikisha wananchi katika kila jambo linalohusu vipaombele vya maeneo yao. 

Kwa upande wao baadhi ya viongozi wa vijiji waliohudhuria katika mkutano huo wamempongeza mkuu wa Wilaya ya Iringa kwa kufanya mkutano uliyolenga kuwakumbusha majukumu yao pamoja na kuwakutanisha kwa pamoja.

Wakati huohuo, watendaji wa vijiji, watendaji wa kati pamoja na watu wa mapato wamekumbushwa kukusanya kodi ikiwemo kodi ya majengo.

Hata hivyo baadhi ya viongozi wa vijiji wamekuwa na wasiwasi kuhusu utekelezaji wa kodi ya majengo kwa kusema wananchi wengi katika maeneo hawana uelewa juu ya kodi hiyo.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mahuninga, Kata ya Mahuninga wilayani Iringa, Lonjino Mkwele alitaka kujua Kodi ya Majengo itatozwaje.

Kwa upande wake, Mdhamini wa Wilaya ya Iringa, John Brayson aliwaomba wananchi wote kulipa kodi ya majengo kwa maendeleo ya uchumi.

Alisema wameanza zoezi kwa kuthamini na ukusanyaji wa kodi ya majengo na mchakataji wa taarifa za majengo umeanza katika jumla ya vijiji 133 vya wilaya pamoja na kata 28.

Brayson alisema kuwa wanapata changamoto katika kutekeleza sheria ya kodi ya majengo hasa maeneo ya vijiji hapo awali walikuwa hawatozwi.

ADHABU KWA ATAKAYESHINDWA KULIPA KODI YA MAJENGO
· Kutozwa faini ya asilimia 50 ya kodi yake.
 
Asipolipa halmashauri imepewa mamlaka ya kukamata mali yenye thamni sawa na kodi na kuuza kufidia kodi hiyo.

Kodi ya majengo katika Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ilianza kutozwa mwaka 1983, katika kipindi hicho kodi hii ilitozwa katika maeneo ya majiji, manispaa, miji midogo na makao makuu ya halmashauri ya wilaya tu.

Lakini mwaka 2015 yalifanyika marekebisho ya sheria kuruhusu hata maeneo mengine ya halmashauri ya wilaya kutoza kodi ya majengo kwa kuthamini majengo kwa njia ya mkupuo.

0 maoni:

Chapisha Maoni