Alhamisi, 19 Januari 2017

HALMASHAURI YA MUFINDI YAPITISHA BAJETI YA BILIONI 60.7 KWA MWAKA WA FEDHA 2017/2018

Posted by Esta Malibiche on JAN 19,2017 IN NEWS
Kikao cha baraza la Madiwani wa halmashauri ya Wilaya ya Mufindi kinaendelea mjini Mafinga muda huu, kwa taarifa zaidi na picha, tembelea na like ukurasa rasmi wa halmashauri ujulikanao kama (mufindi district council)

 Wenyeviti wa kamati za kudumu za halmashauri ya Wilaya ya Mufindi wakipitia kwa umakini makablasha ya bajeti.

 Profesa Riziki Shemdoe Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Mufindi akizungumza mara baada ya kupitishwa kwa bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 yenye jumla ya sh. bilioni 60.7
 Mkuu wa idara ya Fedha wa halmshauri Mr. Mhando akijibu maswali ya madiwani wakati wa kupitia bajeti ya kila idara na vitengo vya halmshauri ya Wilaya ya Mufindi.



 
Na Afisa Habari Mufindi

Baraza maalum la madiwani wa halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, limejadili na kupitisha mapendekezo ya bajeti ya halmshauri hiyo, yenye jumla ya Sh. bilioni 60.7 kwa mwaka wa fedha wa 2017- 2018 huku kiasi kikubwa cha fedha hiyo ikikielekezwa kwenye miradi ya maendeleo.

Taarifa iliyotolewa na kitengo cha habari na mawasilino cha halmshauri ya Wilaya ya Mufindi, imebainisha sehemu kuu mbili za bajeti hiyo, ambapo jumla ya shilingi bilioni 4.9 zimetengwa kwa matumizi ya kawaida, bilioni 41.2 zikibajetiwa kwa ajili ya mishahara ya watumishi wake, wakati bilioni 14.5 zikielekezwa kwenye miradi ya maendeleo.

Taarifa hiyo imevitaja vyanzo vya mapato hayo, kuwa ni makusanyo ya halmashauri, fedha kutoka serikali kuu, wafadhili, taasisi za kijamii sanjari na nguvu za wananchi.

Akizungumza wakati wa kuhailisha kikao hicho, mwenyekiti wa halmshauri ya wilaya ya Mufindi Mh. Festo Mgina amemtaka Mkurugenzi mtendaji pamoja na wataalamu wake kuhakikisha wanaisimamia na kuitetea bajeti kwa hoja zenye mashiko katika ngazi ya Mkoa na Taifa  ili malengo ya kuharakisha maendeleo ya  halmashauri yafikiwe kwa wakati na akawahimiza watumishi na madiwani kushirikiana katika ukusanyaji wa mapato.


Kupitishwa kwa bajeti ya na baraza la madiwani, ni kwa mujibu wa sheria ya fedha yaserikali za mitaa namba 9 ya mwaka 2013. Aidha bajeti hiyo imezingatia mwangozo wa kitaifa wa bajeti wa 2017/ 2018, ilani ya uchaguzi ya chama tawala CCM ya 2015/2020, mpango wa maendeleo wa Taifa wa mwaka 2017/2018 huku mambo mengine yakiwa ni malengo ya maendeleo endelevu, dira ya Taifa ya maendeleo 2025 pamaja na maelekezo ya kisekta  na mpango wa maendeleo ya miaka  mitano.

0 maoni:

Chapisha Maoni