Alhamisi, 19 Januari 2017

HALMASHAURI YA MUFINDI YA YANG”ARA KATIKA UFAULU SHULE ZA MSINGI

Posted by Esta Malibiche on JAN 19,2017 IN NEWS

 
Na Afisa Habari Mufindi                                                                                                 
Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imeendelea kustawi katika sekta ya elimu  ambapo tathimini ya  matokeo  ya darasa la saba  yanaonesha kupanda kutoka asilimia 80.39 mwaka 2015  hadi  asilimia 84.90% mapema mwaka jana, ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 4.51  ikipishana kwa asilimia 03 pekee na mshindi wa kwanza ambaye ni Manispaa ya Iringa mwenye asilimia 87.43.

Taarifa ya Kitengo cha habari na mawasilino cha halmashauri, imetaarifu kuwa, hayo yamebainishwa na ofisa elimu taaluma Bi. MARIAMU NGARA wakati wa kikao cha kila mwaka cha thimini ya elimu ambacho huwakutanisha wakuu wa shule zote za msingi na maaofisa elimu kata, ambapo tathimini ya ufaulu huo umejumuisha shule 143, watahiniwa elfu 05 mianne 38 wavulana wakiwa  elfu 02 miatatu 84 na wasichana ni elfu 03 na 54 huku wanafunzi waliofaulu na kuchaguliwa kuendelea na elimu ya Sekondari  wakiwa ni elfu 4 miasita 17 sawa na asilimia 84.9.

Akisoma taarifa hiyo Bi. NGALA ameainisha masomo ambayo wanafunzi wamefanya vizuri zaidi kuwa ni pamoja na somo la Kiswahili ambalo  ufaulu wake  ni  asilimia 90. 51, Sayansi 90.13, Maarifa 87.88, Hisabati 56.34 huku somo la Kingereza likishika nafasi ya ano kwa asilimia 27.20

Aidha, afisa elimu huyo mwenye dhamana ya taaluma katika Wilaya, ametaja baadhi ya malengo ambayo walijiwekea na ndiyo yaliyochangia kufikia mafanikio hayo kuwa ni pamoja na kufaulisha kwa asilimia 95, ufuatiliaji wa utendaji kazi, uwepo wa kambi za masomo, udhibiti wa utoro wa Wanafunzi na Waalimu, ukamilishaji wa mada kwa wakati na uwepo wa mazoezi ya kujipima.

Idara ya elimu msingi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imeweka uratibu wa kufanya tathimini ya kina kwa kila mwaka mara baada ya kutoka kwa matokeo ya mitihani ya darasa la saba ili kuangazia mafanikio ya ufaulu kwa kila shule, kubainisha changamoto na kuziwekea mikakati ya kuzikabili huku tathimini hiyo ikienda sanjari na kutunuku  zawadi na vyeti kwa wakuu wa shule na maofisa ilimu kata walifaulisha wanafunzi wengi zaidi hivyo kupandisha wasitani wa ufaulu wa halmashauri.

0 maoni:

Chapisha Maoni