Ijumaa, 13 Januari 2017

KIKUNDI CHA WANDISHI WA HABARI CHAPEWA MASHINE YA KUOSHEA MAGARI IRINGA

Posted byEsta Malibiche on JAN 13,2017 in NEWS


Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela amewataka waandishi wa habari kujiunga katika vikundi vya ujasiliamaliili waweze kujiinua kichumi kupotia fursa zitolewazo na taasisi za fedha na mifumo mbalimbali ya umma.
 Kasesela alitoa kauli hiyo  wakati wa hafla fupi ya kukabidhi mashine ya kuoshea magari kwa kikundi cha ujasiliamali cha waandishi wa habari mjini Iringa.
 Akizungumza kwenye hafla hiyo Kasesela alisema waaandishi wamekuwa wakitumiwa na watu wengi ususani viongozi kufukia malengo yao lakini wamekuwa hawana msaada kwao mara baada ya
 kufanikiwa.
 “Mimi nitumie fursa hii kuwashauri waandishi wa habari,ninyi ni nguzo muhimu katika nchi yetu,ni kioo cha jamii nammekuwa chanzo cha mafanikio kwa watu wengi hususani viongozi, lakini niseme tu nimekuwa nikisitishwa na pale watu wanapofanikiwa hushindwa kurudi kuwabeba ninyi”alisema Kasesela.
 Kasesela aliwataka viongozi na makundi ya watu wengine  kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa waandishi wa habari ikiwa ni pamoja na kusaidia vikundi vyao vya ujasimalia ili
 waweze kunufaika na mafanikio yaliyofikiwa.
>Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya alishauriwaandishi na makundi mengine wanapoanza mwaka huu wa 2017 wajenge utamaduni wa kujituma katika kufanya kazi na kuwa na
 shughuli za ziada ili kujiongezea kipato.
 “Tupambane na umasikini,mwaka wa 2016 umeisha yatupasasasa kujitafakari,wapo tulikosea na wapo tumefanikiwa lakini jambo la msingi katika kipindi cha mwaka 2017 nito wito kwenue waandishi na kwa   makundi mengine kufanya kazi kwa bidii na kuwa na shughuli za ziada zenye
 kuwaongezea kipato”alisema Kasesela.
 Awali mwenyekiti wa kikundi hicho Frenk Leonard alimshukuru Mkuu huyo wa Wilaya na kufafanua kuwa mashine hiyo pamoja na mchango wa ununuzi w atangi wa Sh 100,000 aliotoa vitatumika
 kwa mafufaa ya wanakindi.
“Nitumie fursa hii kukushuru wewe kwa moyo wako wa ukarimu,kama miezi miwili iliyopita tulikuja a wazo letunawe hukusita akatutaka tuje na mchanganuo ,tumekuletea na leo umetekeleza,nisema tunakushuru sana na nikuhakikishe mashine hii tutaitumia kwa uadilifu na kwa malengo
 yaliyokusudiwa”alisema Leonard.
Kwa upande wake Tukuswiga Mwaisumbe ambaye ni mwanachama wa kikundi hicho alisema msaada huo umejenga morali kwawanakikundi wa kuendelea kujitafutia kipato  badala ya kutegemea mshahara pekee ambao hautoshi kukidhi mahitaji yakila siku.



0 maoni:

Chapisha Maoni