Ijumaa, 13 Januari 2017

RC IRINGA AAGIZA WALIOKULA FEDHA ZA SACCOS WASAKWE WAKAMATWE

Posted by Esta Malibiche on JAN 13,2017 in NEWS

Mkuu  wa  mkoa  wa Iringa Amina Masenza  akifungua  kikao  cha kamati ya ushauri  ya  mkoa  wa Iringa (RCC)  leo katika  ukumbi wa Siasa ni  Kilimo ,kulia  kwake ni katibu  tawala wa mkoa  wa Iringa Wamoja  Ayubu
Rc  Iringa  akiwa amefika kwa wakati  ukumbini  huku  wajumbe  wengine  wakiwa  bado  kufika
DC  Mufindi  Jamhuri Willium  ,DC  Iringa  Richard Kasesela na Dc  Kilolo Asia Abdalah  wakiwa katika  kikao  cha RCC leo

SERIKALI  ya  mkoa  wa  Iringa  imewaagiza   maofisa  ushirika  wa  vyama  vya  akiba na mikopo  (SACCOS)  kufanya  uchunguzi  na ukaguzi  wa  Saccos  zote  ndani ya wilaya   zao  na  kuwachukulia  hatua kali  viongozi  wa  Saccos  zitakazobainika   kutafuna    fedha  za  wanachama   wake .

Agizo  hilo  limetolewa  leo  na  mkuu  wa  mkoa   wa  Iringa  Amina Masenza  wakati wa  kikao  cha kamati ya  ushauri  ya  mkoa wa Iringa (RCC) kilichofanyika  katika   ukumbi wa Siasa  ni  Kilimo ,  alisema kuwa   zipo  baadhi ya  Saccos  ambazo viongozi   wake  wametafuna  fedha  jambo  ambalo  halitavumilika .

Hivyo  alimwagiza   afisa  ushirika wa  mkoa  wa  Iringa  kufanya  uchunguzi na  ukaguzi  kwa  Saccos  zote  ili  kuzibaini  zile  ambazo  zimetafuna    fedha  za   wanachama   wake  .

“  Ninakuagiza  afisa  ushiriki  wa  mkoa wa  Iringa fanya  ukaguzi  Saccos  zote na  usiache  kuchukua  hatua kali  kwa  viongozi  ambao  watabainika  kutafuna   fedha  za  Saccos”

Katika  hatua  nyingine  mkuu  huyo  wa  mkoa  aliagiza  kuwekwe mkakati  wa  kila  wilaya  wa  kuwalinda  watoto  wa  kike  ambao  wamekuwa  wakikatishwa  masomo kwa  kupewa  mimba  na  watu  wasiopenda  watoto  hao  kusoma.

Kauli  hiyo ya  mkuu  wa  mkoa imekuja  kufuatia  ushauri  uliotolewa na mkuu  wa  wilaya ya  Kilolo Asia Abdalah katika  kikao   hicho  kwa  kuomba  kikao   hicho  kutangaza tatizo la  mimba katika  mkoa  wa  Iringa ni  janga  la  kimkoa  hivyo  kuwekewa  mkakati wa  kupambana na  janga    hilo pamoja na ubakaji  watoto .

Akitoa  maagizo kwenye  kikao  hicho  kufuatia  ushauri  wa mkuu  huyo  wa wilaya ya  Kilolo mkuu wa  mkoa wa Iringa Masenza  alitaka   kila  mmoja  kwa  nafasi yake  kuhakikisha  anapambana na mimba  kwa  wanafunzi  na  pia  kuwataka  wazazi  kuacha mara  moja  tabia ya  kuwatuma  watoto  dukani  ama  maeneo  mengine  usiku .

Huku  akiwaomba  viongozi  wa  dini  zote  mkoani Iringa  kuendelea  kutumia  nyumba  zao  za  ibada  kukemea vitendo vya  ubakaji na mimba kwa  wanafunzi  huku kwa  upande wa  jamii inayowazunguka  aliitaka  kuacha  kuwaficha  watu  wanaoendesha   vitendo vya ubakaji na kuarubuni  wanafunzi  wa  kike .

Katika  kikao   hicho  mbunge  wa Iringa  mjini mchungaji Peter  Msigwa  aliomba  wabunge  wote  wanaotoka  mkoa  wa Iringa  kuungana  kupeleka  hoja  bungeni ya ucheleweshwaji  wa  pesa  kutoka  serikali  kuu  kuja katika  Halmashauri .

0 maoni:

Chapisha Maoni