Jumatatu, 16 Januari 2017

JAFO AONYA UVUVI HARAMU WILAYANI MAFIA

Posted by Esta Malibiche on JAN 16,2017 in NEWS

Naibu Waziri Tamisemi,Seleman Jafo

Na Mwamvua Mwinyi,Mafia

NAIBU Waziri Tamisemi ,Selemani Jafo amemtaka afisa Uvuvi wa halmashauri ya wilaya ya Mafia,mkoani Pwani kuhakikisha anadhibiti uvuvi haramu wa kutumia mabomu na kama uvuvi huo utaendelezwa afisa huyo atawajibishwa.

Sambamba na hayo ameeleza halmashauri ya wilaya ya Mafia hali sio shwari hivyo watendaji wajitume kwa kufuata kasi ya serikali iliyopo madarakani.

Alisema, matumizi ya mabomu yamekua mwiba kwa mazalia ya samaki baharini ambayo madhara yake ni makubwa kwa nyakati zijazo ambayo yanatakiwa kudhibitiwa mapema.

"Nikisikia uvuvi haramu wa kutumia mabomu unaendelea huku samaki wakifa na kupunguza ongezeko, afisa uvuvi kazi hana, kwasababu tunaendelea kutoa maagizo lakini hakuna usimamizi mzuri"alisema Jafo.

Alisema, uvuvi haramu matumizi ya mlipuko na nyavu hazistahili kutumika katika kuvua samaki na ni jambo la hatari.

Aliwataka watendaji kuacha kufanya kazi kwa mazoea  kwani baadhi ya mambo yanaendelea kuzorota kwa kutokua na mabadiliko.

Jafo alisema, athari kubwa itakua kwa kwa watu ambao watashindwa kufuata maelekezo ya viongozi.

Aidha alisema Halmashauri ya wilaya ya Mafia bado hali si nzuri kutokana na utendaji mbovu na kama wapo watendaji wataendelea kutowajibika na kubadilika hatua zitachukulia.

0 maoni:

Chapisha Maoni