Jumapili, 29 Januari 2017

CHAMA CHA MAPINDUZI CCM MKOA WA IRINGA CHAZINDUA SHEREHE YA MIAKA 40 YA KUZALIWA KWAKE

Postedy by Esta Malibiche on JAN 30,2017 IN SIASA

CHAMA cha Mapinduzi ccm Mkoa wa Iringa kimezindua sherehe za miaka 40 tangu kuzaliwa kwake mwaka februari 5,1977.
Sherehe hizo zilifanyika  katika Manispaa ya Iringa na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali.

Chama cha Mapinduzi ccm huadhimisha kila mwaka kuzaliwa kwake,ambapo kwa mwaka 2017 zitafanyika Mkoani Dodoma februari 5.
 Akizungumza katika sherehe hizo, Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi ccm Mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu aliwataka wanaccm kukienzi chama kwa vitendo kwa kufuata nyayo za waasisi.
''Ninawashukuru waasisi wa ccm kuanzia TANU ,Tanzania bara na Zanzibar ,kwasababu waliweza kukitetea chama na kuweka misingi imara hadi hivi sasa kinaendelea kushika atamu''''alisema Msambatavangu
 ''Ingawa  tuko katika mfumo wa vyma vingi lakini     tunaendelea kupambana na kuhakikisha ccm inashika dora''

Awali  katibu wa ccm Iringa Mjini Nuru Ngereja alisoma Historia ya ccm  tangu kuanzishwa kwke na kusema kuwa  Chama cha Mapinduzi ccm kilizaliwa  tarehe 5,februari 1977 kutokana na kuvunjwa kwa vyama vya Tanganyika African Union [TANU] na Afro- Shirazi Part [ASP]
Ngereja alisema Muungano wa TANU na ASP ndio uliowezesha CCM kuwa chama chenye nguvu, imara na madhubuti.Hivyo chama cha siasa chenye uwezo wa hali ya juu ya kuwaunganisha watanzania. 

''''''Poamoja na kwamba Chama cha Mapinduzi kuwa kilizaliwa rasmi tarehe 5 februari,1977,chimbuko lake linaanzia miak mingi kabla,sambama na historia ya uhai wa Taifa la Tanzania.Mzizi ya CCM ya Historia ya CCM imo ndani ya harakati za kukaa ukoloni na usultani,zilizofanyika na wananchi wa Tanzania '''alisema Ngereja





 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu akizungumza katika sherehe ya uzinduzi wa 40 ya kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi zilizofanyika Jumamosi 28,1.2017
















 










0 maoni:

Chapisha Maoni