Jumatatu, 30 Januari 2017

MADINI AINA YA BUNYU YAGUNDULIWA MIKOA YA LINDI NA MTWARA

Posted by Esta Malibiche on JAN30,2017 IN NEWS

Lindi Yetu


.
Machimbo

Na. Ahmad Mmowa, Lindi
Utafiti uliofanyika katika mikoa ya Lindi na Mtwara (kanda ya kusini) umesababisha kugunduliwa kwa mashapo ya madini aina ya bunyu (kinywe) yenye uzito wa tani 689.7 milioni
 Hayo yameelezwa na mhandisi wa migodi wa kanda ya kusini, Aidan Mhando kwenye kongangamano la siku moja la wadau wa mradi wa uchimbaji wa madini ya bunyu katika vijiji vya Namangale, Utimbula vilivyo katika wilaya Lindi na mkoa wa Lindi, Chidya na Chiwata vilivyopo katika wilaya ya Masasi mkoa wa Mtwara. Yaliyofanyika katika manispaa ya Lindi.

Mhandisi Mhando ambae pia ni kaimu kamishna msaidizi wa madini wa kanda ya kusini, alisema kazi ya kuchimba kiasi hicho kilichogunduliwa inakaribia kuanza hivi karibuni.

Kwasababu hatua iliyobaki ni kupata leseni ya uchimbaji baada ya hatua nyingine kukamilika. Aliyataja maeneo ambayo uchimbaji huo utafanyika kuwa ni Namangale, Utimbula, Chiwata na Chidya. Ambapo mitambo mikubwa ya kuchakata itajengwa katika vijiji vya Utimbula na Namangale vilivyopo katika wilaya ya Lindi. Kutokana na uwingi wa madini hayo katika vijiji hivyo.

Alisema soko la bunyu ni zuri na kubwa kutokana na kuzalishwa na nchi chache wakati mahitaji ni makubwa. Akibainisha kwamba wazalishaji wakubwa walikuwa ni nchi ya China. Hata hivyo hivi sasa nchi hiyo haizalishi kwa wingi.
"Kuna haja ya kuanza uchimbaji haraka ili kuwahi soko kutokana na baadhi ya nchi jirani, ikiwamo Msumbiji inatani takribani bilioni mbili za madini hayo," alisema Mhando.

Mhandisi Mhando alizitaja kampuni za kampuni za utafiti ziligundua madini hayo kuwa ni Urinex inyofanya utafiti katika wilaya ya Ruangwa iliyogundua mashapo yenye uzito wa tani 174 milioni, Nachi katika wilaya ya Lindi (tani milioni 446), Lindi jumbo (tani milioni29.6) katika wilaya ya Ruangwa, na Ngwena (tani milioni 25) katika wilaya Ruangwa na Nachingwea.

Mhando alibainisha kuwa kampuni nyingine zinaendelea kufanya utafiti katika wilaya za Nachingwea na Ruangwa. 
Huku akizitaja kampuni hizo kuwa ni Nazareti, Pacco na ASA.

Aidha kaimu kamishna huyo alisema hadi sasa zimeshatolewa leseni ndogo za utafiti 4183 katika mikoa ya Lindi na Mtwara. Ambapo katika mkoa wa Lindi zimetolewa 3625, na Mtwara 558.

Nae mwakilishi wa kampuni ya Nachi, mhamdisi Jimmy Ijumba alisema kampuni hiyo ambayo itachimba madini hayo inatarajia kusafirisha tani 100,000 hadi 180,000 kwa mwaka.

Ijumba alizitaja baadhi ya faida zitakazo patikana kupitia mradi huo pindi uchimbaji utakapoanza kampuni hiyo itawaajiri watu 270. Ambapo watu 220 kati ya hao watakuwa wazawa.
"Mradi utakuwa na faida nyingine, ikiwa ni pamoja na kuvutia uwekezaji mwingi wa huduma na uzalishaji mali ambao utapelekea utengenezaji wa fursa na ajira zaidi kwa wakazi wa maeneo ya mradi," alisema Ijumba.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Masasi, Semani Mzee alitoa wito kwa wawekezaji. Ikiwamo kampuni ya Nachi watumie uzoefu wa utekelezaji wa miradi iliyofanyika ili kuepuka kuwa chanzo cha migogoro kutokana kutolipa fidia kwa wakati kwa wanachi wanaachia maeneo na mali zao kwa ajili ya kupisha miradi mbalimbali.

Ambapo pia alitoa wito kwa wananchi wenye tabia ya kuendeleza maeneo ambayo yameshafanyiwa tathimini kwa lengo la kulipwa fidia kubwa waache tabia hiyo.

Kongamano hilo lililokuwa na lengo kuwajengea uelewa wadau hao kuhusu mradi huo uliwashirikisha pia wawakilishi kutoka kata za Chiwata na Namangale na viongozi wa serikali za vijiji vya Utimbula, Namangale A na B.

0 maoni:

Chapisha Maoni