Jumanne, 4 Oktoba 2016

ULEGA: MUDA WA SASA NI KUFANYA MAENDELEO NA SIO VINGINEVYO.

Posted by Esta Malibiche on Oct4.2016 in SIASA

ul1
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akikagua jengo linalotarajiwa kuwa shule mpya katika kitogoji cha kikonga katika ziara yake kijiji kwa kijiji kwa kushukuu wananchi kwa kumchagua pamoja kuangalia maendeleo leo katika Kijiji cha Bupu Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani.
ul2
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akizungumza na wananchi katika kitongoji cha Kikonga akiwa ziara yake kijiji kwa kijiji kwa kushukuu wananchi kwa kumchagua pamoja na kuangalia maendeleo leo katika Kijiji cha Bupu Wilaya ya Mkuranga.
ul3
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akizungumza katika mkutano wa wananchi wa kitogoji cha Kikonga juu ya changamoto zinazowakabili akiwa ziara yake kijiji kwa kijiji kwa kushukuu wananchi kwa kumchagua pamoja kuangalia maendeleo leo katika Kijiji cha Bupu Wilaya ya Mkuranga.
ul4
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akiwaonyesha wananchi Diwani wao,Abbas Msangule jinsi ya kushirikiana naye kwa maendeleo katika Kijiji cha Kondo Mwelazi katika ziara yake kijiji kwa kijiji kwa kushukuu wananchi kwa kumchagua pamoja kuangalia maendeleo leo katika Kijiji cha Bupu Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani.
ul5
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akiwa katika picha ya pamoja  na walimu wa  shule ya msingi  Kondo Mwelazi alipowatembelea kujua mazingira walionayo  na kuwashukuru kuendelea na moyo licha ya kuwa na mazingira mgumu leo.
…………………………………………………………..
Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega amewataka wananchi kufanya maendeleo na sio siasa kwa muda huu.
Hayo ameyasema leo katika katika ziara ya vijiji vya kata ya bupu, Ulega amesema kuwa wakati umefika kwa kabila yake kusomesha watoto kwa ajili ya maendeleo kutokana dunia ya sasa inahitaji watalaam.
Ulega amesema kuwa changamoto zilizo katika kata ya Bupu ni maji pamoja na miundombinu ya barabara hivyo vinatakiwa kupatiwa ufumbuzi ili wananchi waondokane na changamoto hizo.
Mbunge huyo ameahidi kutoa Bati 50 katika shule mpya inayojengwa katika kitongoji cha kikonga  kutokana watoto wa kitongoji hicho wanatembea kilomita sita.
Ulega amesema changamoto zilizopo wilaya ya mkuranga zinatakiwa zitatuliwe kutokana na kuomba kazi ya kuwatumikia wananchi.
Amesema kuwa suala mfuko wa afya ya jamii CHF dawa hazipatikani na kufanya wananchi wengine washindwe kujiunga.
Aidha amesema wananchi waliojiunga na CHF ni 65 ikiwa nia serikali ni watu wote wajiunge ili wasipate adha ya kupata huduma za afya.
Hata hivyo amesema nia ya Rais Dk. John Pombe Magufuli ni kuona wananchi wanafurahia huduma zinazotolewa na serikali na sio vinginevyo.
 waakuu mdawenu

0 maoni:

Chapisha Maoni