Jumamosi, 13 Agosti 2016

MIFUKO YA BIMA YATAKIWA KUWEKEZA KWENYE VIWANDA

Postedy by Esta Malibiche on August 13.2016 in News

mh1
Waziri wa Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Jenista Mhagama akizungumza na Wakurugenzi  na Watendaji wa Mifuko  ya Hifadhi ya Jamii katika mafunzo kwa bodi za udhamini za mifuko ya hifadhi ya jamii kuhusu uendeshaji na usimamizi wa mifuko ya hifadhi  yaliyoandaliwa na Shirikisho la Mifuko ya hifadhi ya jamii (TSSA) yaliyofanyika jana jijini Arusha.Picha zote na mahmoud ahmad
mh2
Waziri wa Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Jenista Mhagama akizungumza na Wakurugenzi  na Watendaji wa Mifuko  ya Hifadhi ya Jamii katika mafunzo kwa bodi za udhamini za mifuko ya hifadhi ya jamii kuhusu uendeshaji na usimamizi wa mifuko ya hifadhi  yaliyoandaliwa na Shirikisho la Mifuko ya hifadhi ya jamii (TSSA) yaliyofanyika jana jijini Arusha.Picha na mahmoud ahmad
mh3
Mwenyekiti wa Shirikisho la Mifuko ya hifadhi (TSSA) Eliud Sanga akifafanunua jambo katika mafunzo kwa bodi za udhamini za mifuko ya hifadhi ya jamii kuhusu uendeshaji na usimamizi wa mifuko ya hifadhi  yaliyoandaliwa na Shirikisho la Mifuko ya hifadhi ya jamii (TSSA) yaliyofanyika jana jijini Arusha.
mh4
Katibu wa Shirikisho la Mifuko ya hifadhi (TSSA) Meshach Bandawe akizungumza katika Mafunzo hayo.
mh6
Waziri wa Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Jenista Mhagama Akiteta jambo na Mwenyekiti wa Shirikisho la Mifuko ya hifadhi (TSSA) Eliud Sanga  katika mafunzo kwa bodi za udhamini za mifuko ya hifadhi ya jamii kuhusu uendeshaji na usimamizi wa mifuko ya hifadhi  yaliyoandaliwa na Shirikisho la Mifuko ya hifadhi ya jamii (TSSA) yaliyofanyika jana jijini Arusha.Picha na mahmoud ahmad
mh7
Mkurugenzi Mkuu wa PPF William Erio akisikiliza jambo kwa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Profesa Godius Kahyorara.
mh8
Waziri wa Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Jenista Mhagama Akitoa cheti kwa Mjumbe wa Bodi ya PPF kutoka TUCTA Adelgunda Michel aliyeshiriki katika mafunzo kwa bodi za udhamini za mifuko ya hifadhi ya jamii kuhusu uendeshaji na usimamizi wa mifuko ya hifadhi  yaliyoandaliwa na Shirikisho la Mifuko ya hifadhi ya jamii (TSSA) yaliyofanyika jana jijini Arusha.
mh9
Waziri wa Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Jenista Mhagama Akitoa cheti kwa Mjumbe wa Bodi ya LAPF Sarah Mwaipopo
mh10
Waziri wa Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Jenista Mhagama Akitoa cheti kwa Noel Nchimbi Mjumbe wa Bodi ya NSSF
mh11
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mrisho Gambo akizungumza
mh12
Waziri wa Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Jenista Mhagama akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Mafunzo
……………………………………………………………………..
Na Mahmoud Ahmad,Arusha.
Waziri wa Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Jenista Mhagama ameitaka Mifuko ya Hifadhi ya jamii kuwekeza kwenye viwanda ili kuchochea uchumi wa viwanda utakaolisaidia taifa kukua kiuchumi na pia kuwanufaisha wanachama wa mifuko hiyo kutokana na uwekezaji huo wenye tija.
Jenista Amesema hayo akizungumza na Wakurugenzi wa Mifuko pamoja na Watendaji katika mafunzo kwa bodi za udhamini za mifuko ya hifadhi ya jamii kuhusu uendeshaji na usimamizi wa mifuko ya hifadhi  yaliyoandaliwa na Shirikisho la Mifuko ya hifadhi ya jamii (ISSA) .
Amewataka Wakurugenzi hao kuunga mkono Agenda ya taifa ya kulifikisha taifa kwenye uchumi wa kati kupitia viwanda.
Waziri huyo amewataka Wakurugenzi wa mifuko kuhakikisha kuwa wanadhibiti mifuko hiyo ili wanachama waweze kupata mafao yao kwa wakati muafaka bila kuwepo kwa ucheleweshaji.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Mifuko ya hifadhi (ISSA) Eliud Sanga amesema kuwa Shirikisho hilo litaendelea kuhimiza Mifuko hiyo kutimiza wajibu wake katika kutoa mafao bora kwa wanachama wao pamoja na kubuni mafao mapya ili kuwavutia wanachama.
Sanga amesema kuwa kwa sasa mifuko hiyo imefungua milango yake wazi kuwapokea wanachama kutoka sekta ambazo si rasmi ili nao waweze kunufaika na mafao .

0 maoni:

Chapisha Maoni