Mchezaji wa timu ya Yanga
Obrey Chrwa akiwatoka wachezaji wa timu ya Mouloudia Bejaia ya Argeria
kwenye mchezo wa Klabu Bingwa Barani Afrika uliofanyika kwenye uwanja wa
Taifa leo huku Yanga ya Tanzania ikiibuka kwa goli lililofungwa na
Mchezaji wa kimataifa kutoka nchini Burundi, Amisi Tambwe dakika ya
tatu ya mchezo dhidi ya Timu ya Mouloudia Bejaia ya nchini Algeria.
Baada ya ushindi huo Yanga
wanaendea kusalia katika nafasi ya nne wakiwa na alama nne huku mchezo
kati ya Mazembe na Medeama ukitarajiwa kuchezwa kesho nchini Ghana
ukisubiriwa ili kuona kama unaweza kuleta msimamo tofauti wa kundi hilo
baada ya mchezo huo wa kesho.
Mashambulizi golini mwa timu
ya Mouloudia Bejaia yakiendelea timu ya Yanga ilistahili kushinda
magoli mengi lakini washambuliaji wa timu hiyo hawakuwa makini kwani
mipira mingi ilipotelea pembeni mwa milingoti ya goli ama ilidakwa na
golikipa wa timu hiyo.
Mashabiki wa timu ya Yanga wakishangilia wakati mchezo huo ukiendelea kwenye uwanja wa Taifa
0 maoni:
Chapisha Maoni