Postedy by Esta Malibiche on August 12.2016 in News with No comment
Naibu
Waziri Jafo akiwa na Mbunge wa vitimaalum Mkoa wa Shinyanga, Azza Hamad
walipotembelea mradi wa maji ulioanza kutoa maji katika kijiji cha
Tinde Mkoa wa Shinyanga.
Jafo akimtwisha ndoo ya maji mkazi wa kijiji cha Tinde Mkoa wa Shinyanga.
Jafo akizungumza na wananchi na watumishi katika mradi wa maji kijijin cha Tinde.
Naibu Waziri Jafo akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na usalama wa Wilaya ya Shinyanga.
Jafo akikagua barabara mradi wa ujenzi wa barabara za lami katika Manispaa ya Shinyanga zinazojengwa chini ya Tamisemi.
…………………………………………………………………………………………….
NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Tawala
za mikoa na serikali za mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo amewataka wakuu
wa idara kwenye Halmashauri nchini kuacha kufanya kazi kimazoea kwa
kuishia kukaa maofisini bila kwenda maeneo ya vijijini ili kutatua
changamoto zinazowakabili wananchi.
Jafo ametoa kauli hiyo ziara yake
ya kukagua miradi ya maendeleo na kuzungumza na watumishi katika
Halmashauri za Singida, Shinyanga, Uyui na Sikonge mkoani Tabora.
Akizungumza na watumishi katika
halmashauri hizo, Jafo amesema imekuwa ni mazoea kwa wakuu wa idara
kujifungia maofisini bila kufika vijijini kukutana na wananchi ili
waweze kutatua kero zao.
Hata hivyo amewaonya baadhi ya
wakuu wa idara wanaowanyanyasa watumishi wa kada za chini kwa
kuwapendelea baadhi yao katika mchakato wa upandishaji wa madaraja.
Amewaagiza wakurugenzi kupangiana
malengo na wakuu wa idara kuwa ni kitu gani kila mmoja wao atakifanya
ndani ya mwaka mmoja kwenye eneo lake la kazi.
Aidha amesema na wakuu wa idara wafanye hivyo hivyo kwa watu wao wa chini ili kila mtu apimwe kiutendaji ndani ya mwaka mmoja.
Jafo amekemea tabia ya wakurugenzi
wa Halmashauri kupitisha malipo ya miradi ambayo inakuwa imejengwa
chini ya kiwango na kwamba ni ubadhirifu wa fedha za wananchi kwa kuwa
haifikii malengo yaliyokusudiwa.
“Hali kama hii imejitokeza kule
halmashauri ya kondoa mkoani Dodoma serikali imefanya uchunguzi na
tayari hatua zimechukuliwa kwa watendaji 8 ambao wamesimamishwa kazi na
wengine kufikishwa mahakamani kutokana na ubadhirifu wa fedha za miradi
ya maendeleo…Serikali itaendelea kuchukua hatua kwa yeyote atakayefanya
vitendo kama hivi,”amesema Jafo
Naibu Waziri huyo kwa takriban
wiki mbili amefanikiwa kutembelea halmashauri 15 na kutembelea miradi 63
ikiwemo miradi ya hospitali, vituo cha afya na zahanati, miradi ya
elimu, maji, na miundombinu ya barabara.
Miongoni mwa Halmashauri
alizozitembelea ni pamoja na Halmashauri ya Kilolo, Mufindi, Mafinga,
Iringa, Chemba, Kibaha, Korogwe mji, Halmashauri ya Korogwe, Jiji
Arusha, Kisarawe, Singida, Manispaa ya Shinyanga, Halmashauri ya
Shinyanga, Uyui, na Sikonge .
Jafo bado anaendelea na ziara yake katika mikoa ya Katavi na Rukwa kwa lengo kutimiza matakwa ya watanzania.
0 maoni:
Chapisha Maoni