Jumamosi, 13 Agosti 2016

COMFORT ZONE watoa Msaada Kwa yatima wa Kituo cha Hasene Mjini Dodoma

Baadhi ya wanachama wa Comfort Zone waliopo Dodoma wakitoa misaada mbalimbali kwa watoto yatima wanaoishi katika kituo cha kulelea watoto yatima cha Hasene kilichopo eneo la Chang'ombe wilaya ya Dodoma mjini.

Misaada iliyotolewa ni vitu mbalimbali ikiwemo mifuko 20 ya saruji kwa ajili ya kusaidia ukamilishaji wajenzi wa madarasa na bweni la kulala watoto.
Wanachama wa Comfort Zone wakiwa wamebeba baadhi ya Misaada kabla ya kuikabidhi kwa Watoto yatima wa kituo cha Hasene kilichopo eneo la Chang'ombe wilaya ya Dodoma Mjini.
Wanachama wa Comfort Zone wakiwa wameketi na Watoto yatima Baada ya Kuwakabidhi Misaada mbalimbali kwa ajili ya kuwasaidia. 

0 maoni:

Chapisha Maoni