Alhamisi, 11 Agosti 2016

WAZIRI NAPE:SIJAUZUIA KURIPOTI STORI ZA MAANDAMANO TUMEZUIA HABARI ZA UCHOCHEZI

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo NAPE NNAUYE, amelifungia Gazeti la Mseto kwa Miezi 36 kutokana na kuchapisha Habari za Uongo na kugushi kwa kutumia nyaraka mbalimbali za Serikali.

Uamuzi huo wa kulifungia Gazeti hilo umetolewa kwa Tangazo la Serikali Namba 242 lilitolewa jana kwa mujibu wa Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 Sura ya 229, Kifungu 25(1).

Waziri NAPE ameeleza kuwa Kifungu hicho kinampa Mamlaka Waziri kuchukua uamuzi wa kufungia Gazeti kutokana na mwenendo wa uandishi wa Gazeti hilo wa kuandika na kuchapisha habari za uongo na Kugushi kwa kutumia nyaraka mbalimbali za Serikali.

Amefafanua kuwa Serikali kwa masikitiko makubwa imelazimika kilifungia Gazeti la Mseto kutokana na mwenendo wa uandishi wa kuandika na kuchapisha habari za uongo na kugushi.

Ameongeza kuwa Serikali ya Tanzania imeridhia mikataba mbalimbali ya Kimataifa inayoanisha Uhuru wa Habari na mipaka ya Habari ikiwemo tamko la Haki za Binaadamu la mwaka 1948.


Gazeti la Mseto limezuiwa kuchapishwa katika njia nyingine yeyote ikiwemo mitandao kwa mujibu wa Sheria ya MawasiliMsikilize Waziri Nape hapa

0 maoni:

Chapisha Maoni