Ijumaa, 12 Agosti 2016

MBUNGE WA CHALINZE RIDHIWANI KIKWETE AKABIDHI MADAWATI 537 KWA JIMBO HILO

Mbunge jimbo la Chalibze Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani Ridhiwani Kikwete akikabidhi madawati 537 yaliyotolwa na Ofisi ya Bunge ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anamkabidhi dawati Diwani wa Kata ya Msata Selestine Semono.

Ridhiwani Kikwete anamkabidhi madawati Diwani wa Kata ya Ubena Nicholaus Muyuwa. Picha na Mpiga picha Wetu.



Picha za mbali mbali za tukio hilo la ugawaji wa madawati 537 yaliyotolewa na Ofisi Ya Bunge Tanzania kwa Shule zenye upungufu wa madawati.

Madawati hayo yalitolewa katika shule za Jimbo hilo kwa utaratibu kwa kila shule kupata idadi ya madawati yake,shule ya Chalinze madawti 50,Bwilungu 50,Bwilungu B 50,Kikaro 50,Mdaula 50,Msanga 50,shule ya Msigi 7.

Shule nyingine zilizopata madawati hayo ni Msata 15,Pongwe Mwezi 40,Kikwazu 10,Kibundu madawati 50,Mboga19,Mbewe 31,Ruvu Darajani 25 na shule ya Lulenge madaati 10.  

Aidha kutokana na mgao wa madawati hayo jimbo hilo la Chalinze halina tena upungufu wa madawati bali linahitaji kuongeza vyumba vya madarasa

0 maoni:

Chapisha Maoni