Jumapili, 7 Agosti 2016

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI MWIGULU NCHEMBA ALIAGIZA JESHI LA MAGEREZA MKOANI IRINGA KUHAMISHA GEREZA KUU


Postedy by Esta Malibiche in August 7.2016 in KITAIFA with No comment

Na Esta Malibiche
Iringa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu  Nchemba ameagiza uongozi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Iringa kuanza mara moja mchakato wa kuhamisha Gereza kuu la mkoa kutoka katika mji na kwenda pembezoni mwa mji.

Gereza hilo lililopo katika kata ya Miomboni lipo katika kati ya mji na jirani na Hosptali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa na uwepowake umelalamikiwa na wakazi wa mji huo wanaodai umekuwa ukiwakwamisha kufikisha wagonjwa hospitalini kutokana na barabara hiyo kufungwa nyakati za usiku kwa sababu za kiusalama.

Akizungumza mara baada ya kufanya ziara ya siku moja mkoani hapa na kutembelea eneo hilo kujionea hali halisi Nchemba aliuagiza uongozi wa gereza  kuanza mchakato wa kulihamisha gereza hilo lililopokata ya Miyomboni Kitanzini na kulipeleka katika katikakata ya Kwa kilosa lilipogereza dogo la  Mlolo.

“Nimekuja baad aya kusikia kuna malalamiko nikaona nijenitembeleleenione eneolamgogoro ni lipi,nimefika eneohilonakujionea ni kweli pale pamebanana,gereza ingawaje limejaa kuptiakiasi hakuna eneo la kufanyiaupanuzi wakati huo huophosptali wanaotakiwakujenga kitengo cha dharura hawana eneo la kufanyia upanuzi”alisema Nchemba na kuongeza:

‘Kutokana na sababu hizo na kwakuwa Gereza wanaeneo pembezeno ambalo ni kubwa na lipo umbali wa km 7 ninaagiza uongozi wa gereza hili la Mkoa  kuanza mchakato wa ujenzi wa Gereza hilojipya kwa kuchambua wafumgwa waliopo kupata idadi ya wale wenyeuwezo wa  kufanya kazi ili watumeke kwenye ujenzi huo”alisema.

Nchemba aliagizo uongozi huo uchambuziwa wafungwa waliopokatika gereza hilowenye uwezo wa kufanya kaziufanyike sambamba na kazi ya kubaini vifaa vinavyotakiwa katikakazi ya kufyatua tofali vikiwamo vibao vya kufyatulia tofali ilikazi ya ujenzi wa Gereza hiloianze mara moja.

Alisema hatua hiyo pia itasaidia kuondoa msongamano wa wafungwa waliopo katika gereza la mkoa ambao ni katiya 450 na 500 ilehali gereza hilo linauwezo wa kuhifahdi wafungwa 220 tu jambo alilodai nimuhimu kulihamishie kwenye eneo la Kwakilosa lenye ukumbwa wa  hekta 325.

Katika hatua nyinjgine Waziri huyo aliwaeleza wafanyakazi waliopo chini ya Wizara yake ambao ni askari Magereza,Polisi,Uhamiaji na asakari wa zimamoto kuwa na subira wakati malalamiko yao yanayohusiana na posho za nyumba,Kuongeza Nyumba za askari na  sare za askari na kwamba serikali itayafanyia kazi.

Awali akitoa taraifa ya Mkoa huo mbele ya Waziri, Kaimu Mkuu Mkoa wa Iringa Richard Kasesela alisema kuwa changamoto inayowakabili wakaziwa Iringa ni kufungwa kwa barabara inayokwenda katika Hosptali ya Rufaa ikipitia eneo la gereza kuu la mkoa.
Alisema kutokana na malalamiko ya wananchi hao,serikali mkoani hapa imefutalia jambo hilo kwa muda mrefu bila ya mafanikio.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Iringa Mjini Abed Kiponza alimtaka waziri huyo kuamuru kuondolewa  ukuta huo uliojengwa na uongozi wa gereza hilo uvunjwe ili kuruhusu gari kupitisha wagonjwa katika eneo hilo na wananchi wanaoenda kuwaangalia wagonjwa waondokane na adha iliyokuwa ikiwakabili.
“Kufungwa kwa barabara hii kumesababisha matatizomakubwa kwa wananchi wetu tumepoteza maisha yawagonjwa katiya sitanasababu kutokana na kuchelewa kuwafikisha wagonjwa kwenye  huduma,tunaomba Mheshimiwa Waziri utusaidie katika hili”alisema Kiponza.
mwisho






waziri wa mambo ya ndani ya nchi  Bw  Mwigulu Nchemba akisalimiana na  waziri wa nyumba na maendeleo ya makazi Bw  Wiliam Lukuvi (kuli)  leo  baada ya  kukutana  ofisi ya mkuu wa mkoa  wa Iringa
Waziri Lukuvi katikati  akimtambulisha  mkuu wa wilaya ya  Iringa Richard Kasesela kwa waziri Nchemba leo
Waziri Nchemba  akisikiliza jambo  kutoka kwa waziri Lukuvi
Kamanda  wa  polisi wa mkoa wa Iringa Bw  Peter Kakamba  akisalimiana na waziri wa mambo ya  ndani ya nchi Bw Nchemba
Mbunge  Msigwa akisalimiana na waziri wa mambo ya ndani ya nchi Bw Mwigulu Nchemba
Mbunge  wa Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa wa pili kushoto  wakisalimiana  kwa  furaha na  mwenyekiti wa CCM Iringa mjini Abeid Kiponza  huku waziri wa mambo ya ndani ya nchi  Bw Mwigulu Nchemba na  mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela  (kushoto)  wakiangua  kicheko

Waziri Nchemba  akitembelea  eneo la Hospitali ya  Rufaa ya mkoa wa Iringa
Mganga  mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Salmu Robart akimwonyesha  waziri Nchemba ufinyu wa eneo la  Hospitali  hiyo ya rufaa ya mkoa wa Iringa

0 maoni:

Chapisha Maoni