Kamanda wa jeshi la zima
moto na uokoaji mkoani Pwani, mrakibu msaidizi,Goodluck Zerote
,akichangia damu ,katika zoezi lililoendeshwa na jeshi hilo ,kuchangia
damu hospital ya rufaa ya Tumbi.(Picha na Mwamvua Mwinyi)
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
WATOTO chini ya umri wa miaka mitano mkoani Pwani wako kwenye hatari ya kupoteza maisha kutokana na ukosefu wa damu.
Hayo yalielezwa
na afisa muuguzi wa wa kitengo cha damu salama hosptali ya rufaa ya
Tumbi ,Elisia Towo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya
zoezi la utoaji damu kwa hiari lililokuwa likiendeshwa na jeshi la zima
moto na uokoaji mkoani hapo.
Alisema watoto
wenye umri huo wamekuwa wakiongoza kwa kukosa damu kutokana kuugua
ugonjwa wa malaria lakini pia kucheleweshwa kuwahishwa hospitali mapema.
"Tumekuwa
tukiwahamasisha wazazi katika mihadhara mbalimbali kuhakikisha
wanawawahisha watoto hosptali pindi wanapoona dalili ya homa ama
malaria badala ya kuwaleta wakiwa wameshachoka na ugonjwa”, alisema
Towo.
Alieleza kuwa
kundi jingine lililo hatarini ni wakina mama wajawazito ambao nao
wamekuwa wakipata tatizo la ukosefu wa damu ama wakihitaji kufanyiwa
upasuaji .
Towo amesema watu wengine ni majeruhi wa ajali ambao hawatabiriki kwani ajali hutokea bila ya kuwa na taarifa.
Muuguzi huyo
alisema kutokana na mahitaji hayo hosptali ya rufaa ya Tumbi inahitaji
damu nyingi zaidi ambapo kwa sasa iliyopo ni unit 25 ambayo ni ndogo
ikilinganishwa na matukio ya mara kwa mara ya ajali.
“Kwa siku
tunakusanya unit 12 hadi 20 na mahitaji yetu kwa mwezi ni kuanzia unit
250 hadi 300, bado damu haitoshi, nawaomba wananchi wa mkoa wa Pwani
wajitokeze kuchangia damu kwa hiari ili waweze kuokoa maisha ya
watanzania wenzetu wanaohitaji damu”, alisema Towo.
Afisa uhusiano
wa jeshi la zima moto na uokoaji SGT Harrison Mkonyi alisema zoezi hilo
ni endelevu na kuwa lengo ni kuhakikisha jeshi hilo linatimiza kauli
mbiu yake ya kuokoa maisha na mali kwa vitendo.
Kamanda wa
jeshi la zimamoto na uokoaji mkoani Pwani Mrakibu msaidizi Gudluck
Zerote ,alisema hii ni mara ya kwanza kwa jeshi hilo mkoani humo
kuchangia damu.
Kamanda Zerote
alisema kutokana na kuwa kwa mara ya kwanza wamechangia damu hosptali
ya Tumbi unit 12, na kuwa watachangia baada ya miezi mitatu.
0 maoni:
Chapisha Maoni