Jumanne, 9 Agosti 2016

MWIGULU ATEMBELEA KAMBI YA WAKIMBIZI YA KATUMBA NA MISHAMO MKOANI KATAVI

Postedy by Esta Malibiche on August 9.2016 in KITAIFA with No comment





WAZIRI wa mambo ya ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama  kuweachukulia hatua wale wote wanaojihusisha na vitendo vya kibaguzi baina ya wakimbizi
Akizungumza katika kambi ya wakimbizi ya katumba mkoani katavi mapema leo hii wakati akifanya ukaguzi na kuhakiki katika kambi hiyo alisema kuwa  Tanzania hatua tabia za kibaguzi,moja kati ya sifa kubwa ya nchi yetu ni kushinda vita dhidi ya ubaguzi wa aina yoyote tangu tulipopata uhuru.

 Zoezi hiilo  la uhakiki limefanyika ,kutokana na kuwepo kwa  taarifa za baadhi yawakimbizi waliopo katika kambi hizo kujihusisha na watu waovu,,kufanya vitendo vya kibaguzi, na kutoka nje ya kambi zao  kwenda nchi jirani bila kibali.

Aidha  Mbali na kambi ya katumba,pia alitembelea kambi ya Mishamo.Pia aliviagiza vyombo vya usalama na kupitia serikali za mitaa kuwachukulia hatua watu wanaojihusisha na vitendo hivyo.

 '''''Natoa rai kwa raia wote tuliowapa kibali cha kufanya kazi,kuishi na kuwa raia wa nchi yetu, waache kujihusisha na vitendo viovu na vyakibaguzi.Hatutawavumilia watu ambao tumewakaribisha kwa nia njema hapa nchini na baadae wahatarishe usalama na amani ya nchi yetu.'''''alisema Mwigulu

 '''''Vilevile nimekutana na askari wetu wa jeshi la polisi na idara zake zote na nimetembelea gereza la mpanda ikiwa ni ziara ya kupata uhalisia wa changamoto zinazolikabili jeshi la polisi,magereza,uhamiaji na zimamoto kwa kila mkoa,tayari kwa majawabu ya kudumu.'''''alisema Mwigulu

"usalama wetu,jukumu letu sote"









 
Add caption





Picha na Festo Sanga





0 maoni:

Chapisha Maoni